Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Yeremia 47:4 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

4 kwa sababu ya siku ijayo kuwaangamiza Wafilisti wote, kukatilia mbali kila msaidizi wa Tiro na Sidoni asaliaye; maana BWANA atawaharibu Wafilisti, mabaki ya kisiwa cha Kaftori.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

4 Hiyo ni siku ya kuwaangamiza Wafilisti wote, kukomesha msaada uliobakia kutoka Tiro na Sidoni. Maana Mwenyezi-Mungu anawaangamiza Wafilisti, watu waliosalia wa kisiwa cha Kaftori.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

4 Hiyo ni siku ya kuwaangamiza Wafilisti wote, kukomesha msaada uliobakia kutoka Tiro na Sidoni. Maana Mwenyezi-Mungu anawaangamiza Wafilisti, watu waliosalia wa kisiwa cha Kaftori.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

4 Hiyo ni siku ya kuwaangamiza Wafilisti wote, kukomesha msaada uliobakia kutoka Tiro na Sidoni. Maana Mwenyezi-Mungu anawaangamiza Wafilisti, watu waliosalia wa kisiwa cha Kaftori.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

4 Kwa maana siku imewadia kuwaangamiza Wafilisti wote na kuwakatilia mbali walionusurika wote ambao wangeweza kusaidia Tiro na Sidoni. Mwenyezi Mungu anakaribia kuwaangamiza Wafilisti, mabaki toka pwani za Kaftori.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

4 Kwa maana siku imewadia kuwaangamiza Wafilisti wote na kuwakatilia mbali walionusurika wote ambao wangeweza kusaidia Tiro na Sidoni. bwana anakaribia kuwaangamiza Wafilisti, mabaki toka pwani za Kaftori.

Tazama sura Nakili




Yeremia 47:4
27 Marejeleo ya Msalaba  

Kanaani akamzaa Sidoni, mwanawe wa kwanza, na Hethi,


na Wapathrusi, na Wakasluhi; huko ndiko walikotoka Wafilisti, na Wakaftori.


Mungu haondoi hasira zake; Hao wamsaidiao Rahabu huinama chini yake.


BWANA atamcheka, Maana ameona kwamba siku yake inakuja.


Nanyi mtafanya nini siku ya kujiliwa, na wakati wa uangamivu, utakaokuja kutoka mbali sana? Je! Mtamkimbilia nani mpate msaada? Na utukufu wenu mtauacha wapi?


Piga yowe, Ee lango; lia, Ee mji; Ee Ufilisti enyi wote, umeyeyuka kabisa; Maana moshi unakuja toka kaskazini, Wala hakuna atakayechelewa katika majeshi yake.


Na mwenyeji wa nchi ya pwani atasema katika siku hiyo, Angalia, haya ndiyo yaliyowapata watu wale tuliowatumainia, ambao tuliwakimbilia watuokoe kutoka kwa mfalme wa Ashuru; na sisi je! Twawezaje kupona?


Ndipo huyo Mwashuri ataanguka kwa upanga ambao si wa mtu; na upanga usio upanga wa mtu utamwangamiza; naye ataukimbia upanga, na vijana wake watatoa kodi.


Maana hiyo ni siku ya Bwana, BWANA wa majeshi, Siku ya kisasi, ili ajilipize kisasi juu ya adui zake; Nao upanga utakula na kushiba, Utakunywa damu yao hata kukinai; Maana Bwana, BWANA wa majeshi, ana sadaka yake Katika nchi ya kaskazini karibu na mto Frati.


Na wewe, Ewe mtu mwovu, uliyetiwa jeraha kiasi cha kukuua, mkuu wa Israeli, ambaye siku yako imekuja, katika wakati wa uovu wa mwisho;


wakati wanapokupa maono ya udanganyifu, wakati wanapokuagulia uongo, wanakuweka juu ya shingo zao wachukizao, na waovu, ambao siku yao imekuja, katika wakati wa adhabu ya mwisho.


kwa sababu hiyo, Bwana MUNGU asema hivi; Tazama, nitanyosha mkono wangu juu ya Wafilisti, nami nitawakatilia mbali Wakerethi, na kuwaharibu wabakio pande za pwani.


Nao watajua ya kuwa mimi ndimi BWANA, nitakapoweka moto katika Misri, na hao wote wamsaidiao watakapoangamia.


Majira yamewadia, siku ile inakaribia; huyo anunuaye asifurahi, wala asihuzunike auzaye; maana ghadhabu imewapata watu wote.


Siku za kupatilizwa zimekuja, siku za kulipa zimefika; Israeli atayajua hayo; huyo nabii ni mpumbavu, huyo mtu mwenye roho ana wazimu; kwa sababu ya wingi wa uovu wako, na kwa sababu uadui umekuwa mkubwa.


Je! Ninyi si kama wana wa Wakushi kwangu mimi, enyi wana wa Israeli, asema BWANA? Je! Mimi sikuwapandisha Israeli toka nchi ya Misri, na Wafilisti toka Kaftori, na Washami toka Kiri?


Kwa kuwa siku hizo ndizo za mapatilizo, ili yatimizwe yote yaliyoandikwa.


na Waavi waliokuwa wakikaa katika vijiji mpaka Gaza waliangamizwa na Wakaftori waliotoka Kaftori, na hawa wakakaa badala yao.)


Basi Finehasi kuhani, na wakuu wa mkutano, na hao vichwa vya maelfu ya Israeli waliokuwa pamoja naye, hapo walipoyasikia hayo maneno waliyoyasema hao wana wa Reubeni, na wana wa Gadi, na wana wa Manase, maneno hayo yaliwaridhisha sana.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo