Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Yeremia 47:3 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

3 Kwa sababu ya kishindo cha kukanyaga kwa kwato za farasi wake walio hodari, kwa sababu ya mwendo wa mbio mbio wa magari yake ya vita; kwa sababu ya mngurumo wa magurudumu yake, hao akina baba hawatazami nyuma ili kuwaangalia watoto wao, kwa kuwa mikono yao ni dhaifu;

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

3 Watasikia mshindo wa kwato za farasi, kelele za magari ya vita, na vishindo vya magurudumu yao. Kina baba watawasahau watoto wao, mikono yao itakuwa imelegea mno.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

3 Watasikia mshindo wa kwato za farasi, kelele za magari ya vita, na vishindo vya magurudumu yao. Kina baba watawasahau watoto wao, mikono yao itakuwa imelegea mno.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

3 Watasikia mshindo wa kwato za farasi, kelele za magari ya vita, na vishindo vya magurudumu yao. Kina baba watawasahau watoto wao, mikono yao itakuwa imelegea mno.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

3 kwa sauti ya kwato za farasi wanaoenda mbio, kwa sauti ya magari ya vita ya adui, na mngurumo wa magurudumu yake. Baba hawatageuka kuwasaidia watoto wao, mikono yao italegea.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

3 kwa sauti ya kwato za farasi waendao mbio, kwa sauti ya magari ya adui na mngurumo wa magurudumu yake. Baba hawatageuka kuwasaidia watoto wao, mikono yao italegea.

Tazama sura Nakili




Yeremia 47:3
14 Marejeleo ya Msalaba  

Mishale yao ni mikali, na pinde zao zote zimepindika; Kwato za farasi wao zitahesabika kama gumegume; Na gurudumu zao kama kisulisuli;


Haya! Pandeni, enyi farasi; Jihimizeni, enyi magari ya vita; Mashujaa nao na watoke nje Kushi na Puti, watumiao ngao; Nao Waludi, washikao uta na kuupinda.


Wanashika upinde na mkuki; Ni wakatili, hawana huruma; Sauti yao inanguruma kama bahari, Nao wamepanda farasi; Kila mmoja amejipanga kama aendaye vitani, Juu yako, Ee binti Babeli.


Kutoka Dani kumesikiwa mkoromo wa farasi wake; nchi yote pia inatetemeka kwa sauti ya mlio wa farasi wake wa vita; maana wamekuja, wamekula nchi na vyote vilivyomo; huo mji na wote wakaao ndani yake.


Nao watakuja kwako na silaha zao, na magari ya vita, na magurudumu, na wingi wa mataifa; watajipanga juu yako kwa ngao, na vigao, na chapeo za shaba, pande zote; nami nitawapa uwezo wa kuhukumu, nao watakuhukumu kulingana na hukumu zao.


Magari ya vita yanafanya vishindo njiani, Yanasonganasongana katika njia kuu; Kuonekana kwake ni kama mienge, Yanakwenda upesi kama umeme.


Lakini Ninawi tokea zamani amekuwa kama ziwa la maji; ila hata sasa wanakimbia; Simameni! Simameni! Lakini hapana hata mmoja atazamaye nyuma.


Nao walikuwa na dirii kifuani kama dirii za chuma. Na sauti ya mabawa yao ilikuwa kama sauti ya magari, ya farasi wengi waendao kasi vitani.


Kisha, kwa kishindo kwato za farasi zilipigapiga, Kwa maana walivyoenda shoti, Walipowakimbiza farasi wenye nguvu.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo