Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Yeremia 23:40 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

40 nami nitaleta juu yenu aibu ya milele, na fedheha ya daima, ambayo haitasahauliwa.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

40 Nitawaletea fedheha ya milele na aibu ya kudumu ambayo haitasahaulika.”

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

40 Nitawaletea fedheha ya milele na aibu ya kudumu ambayo haitasahaulika.”

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

40 Nitawaletea fedheha ya milele na aibu ya kudumu ambayo haitasahaulika.”

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

40 Nitaleta juu yako fedheha ya kudumu: yaani aibu ya kudumu ambayo haitasahaulika.”

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

40 Nitaleta juu yako fedheha ya kudumu: yaani aibu ya kudumu ambayo haitasahaulika.”

Tazama sura Nakili




Yeremia 23:40
10 Marejeleo ya Msalaba  

Lakini BWANA yuko pamoja nami, mfano wa shujaa mwenye kutisha; kwa hiyo hao wanaonionea watajikwaa, wala hawatashinda; watatahayarika sana. Kwa sababu hawatafaulu wataona aibu ya milele, ambayo haitasahauliwa kamwe.


Naam, nitawatoa watupwe huku na huko katika falme zote za dunia, wapate mabaya; wawe kitu cha kulaumiwa, na mithali, na dhihaka, na laana, katika mahali pote nitakapowafukuzia.


Maana BWANA wa majeshi Mungu wa Israeli, asema hivi, Kama hasira yangu, na ghadhabu yangu, ilivyomwagwa juu ya hao wakaao Yerusalemu, ndivyo ghadhabu yangu itakavyomwagwa juu yenu, mtakapoingia Misri; nanyi mtakuwa apizo, na ajabu, na laana, na aibu; wala hamtapaona mahali hapa tena.


Wewe nawe, ichukue aibu yako mwenyewe, kwa kuwa umetoa hukumu juu ya dada zako; kwa dhambi zako ulizozitenda, zilizochukiza kuliko hao, wao wana haki kuliko wewe; naam, ufedheheke wewe nawe, ukaichukue aibu yako, kwa kuwa umewapa haki dada zako.


Tena, wengi wa hao wanaolala katika mavumbi ya nchi wataamka, wengine wapate uzima wa milele, wengine aibu na kudharauliwa milele.


Ee Bwana sawasawa na haki yako yote, nakusihi, hasira yako na ghadhabu yako zigeuzwe na kuuacha mji wako Yerusalemu, mlima wako mtakatifu; maana kwa sababu ya dhambi zetu, na maovu ya baba zetu, Yerusalemu na watu wako wamepata kulaumiwa na watu wote wanaotuzunguka.


Kadiri walivyozidishwa, kwa kadiri iyo hiyo walinitenda dhambi; nami nitageuza utukufu wao kuwa aibu.


Nawe utakuwa ushangao, na mithali, na dharau, kati ya mataifa yote huko atakakokuongoza BWANA.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo