Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Yeremia 13:22 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

22 Nawe ukisema moyoni mwako, Mbona mambo haya yamenipata mimi? Ni kwa sababu ya wingi wa uovu wako, marinda yako yamefunuliwa, na visigino vya miguu yako vimeumia.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

22 Nawe utajiuliza moyoni mwako, “Kwa nini mambo haya yamenipata?” Sawa! Kama vazi lako limepandishwa juu, nawe ukatendewa kwa ukatili mno, hayo ni matokeo ya makosa yako mengi mno.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

22 Nawe utajiuliza moyoni mwako, “Kwa nini mambo haya yamenipata?” Sawa! Kama vazi lako limepandishwa juu, nawe ukatendewa kwa ukatili mno, hayo ni matokeo ya makosa yako mengi mno.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

22 Nawe utajiuliza moyoni mwako, “Kwa nini mambo haya yamenipata?” Sawa! Kama vazi lako limepandishwa juu, nawe ukatendewa kwa ukatili mno, hayo ni matokeo ya makosa yako mengi mno.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

22 Nawe ukijiuliza, “Kwa nini haya yamenitokea?” Ni kwa sababu ya dhambi zako nyingi marinda yako yameraruliwa na mwili wako umetendewa vibaya.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

22 Nawe kama ukijiuliza, “Kwa nini haya yamenitokea?” Ni kwa sababu ya dhambi zako nyingi ndipo marinda yako yameraruliwa na mwili wako umetendewa vibaya.

Tazama sura Nakili




Yeremia 13:22
24 Marejeleo ya Msalaba  

vivyo hivyo mfalme wa Ashuru atawachukua uchi, wafungwa wa Misri, na watu wa Kushi waliohamishwa, watoto kwa wazee, bila viatu, matako yao wazi, Misri iaibishwe.


Basi, kwa hiyo, Bwana atawapiga binti za Sayuni kwa pele za utosini, na BWANA ataifunua aibu yao.


Sasa, basi, sikia haya, wewe upendaye anasa, ukaaye na kujiona salama, wewe usemaye moyoni mwako, Mimi ndiye, wala hapana mwingine zaidi yangu mimi; sitaketi kama mjane, wala sitajua kufiwa na watoto;


Kwa ajili ya hayo, mimi nami nitayafunua marinda yako mbele ya uso wako, na aibu yako itaonekana.


Na watu hao, waliopewa unabii na wao, watatupwa nje katika njia kuu za Yerusalemu kwa sababu ya upanga na njaa; wala hawatakuwa na mtu wa kuwazika, wao na wake zao, na wana wao, na binti zao; maana nitamwaga uovu wao wenyewe juu yao.


Tena itakuwa mtakapouliza, BWANA ametutenda mambo hayo yote kwa sababu gani? Ndipo utakapowaambia, Vile vile kama ninyi mlivyoniacha mimi, na kuwatumikia miungu mingine katika nchi yenu wenyewe, ndivyo mtakavyowatumikia wageni katika nchi isiyo yenu.


Yerusalemu amefanya dhambi sana; Kwa hiyo amekuwa kama kitu kichafu; Wote waliomheshimu wanamdharau, Kwa sababu wameuona uchi wake; Naam, yeye anaugua, Na kujigeuza aende nyuma.


Pia watakuvua nguo zako, na kukunyang'anya johari zako uzuri.


Naye Efraimu alisema, Kweli nimekuwa tajiri, nimejipatia mali nyingi; katika kazi zangu zote hawataona kwangu uovu wowote uliokuwa dhambi.


Na sasa nitaifunua aibu yake mbele ya macho ya wapenzi wake, wala hapana mtu atakayemwokoa katika mkono wangu.


nisije nikamvua nguo zake akawa uchi, nikamweka katika hali aliyokuwa nayo siku ya kuzaliwa kwake, na kumfanya kama jangwa, na kumweka kama nchi kame, na kumwua kwa kiu;


Maana mama yao amezini; yeye aliyewachukua mimba ametenda mambo ya aibu; maana alisema, Nitafuatana na wapenzi wangu, wanipao chakula changu na maji yangu, sufu yangu na kitani yangu, mafuta yangu na vileo vyangu.


Tazama, mimi ni juu yako, asema BWANA wa majeshi; nami nitayainua marinda yako mbele ya uso wako; nami nitawaonesha mataifa uchi wako, na falme aibu yako.


Kisha itakuwa wakati ule, nitauchunguza Yerusalemu kwa taa; nami nitawaadhibu watu walioganda juu ya masira yao; wasemao katika mioyo yao, BWANA hatatenda mema, wala hatatenda mabaya.


Nawe ukisema moyoni mwako, Tutajuaje neno asilolinena BWANA?


Nawe kama ukisema moyoni mwako, Mataifa haya ni mengi kuliko mimi; nitawatoaje katika milki yao?


Hapo usiseme moyoni mwako, Nguvu zangu na uwezo wa mkono wangu ndio ulionipatia utajiri huo.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo