Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Wimbo Ulio Bora 4:13 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

13 Machipuko yako ni bustani ya komamanga, Yenye matunda mazuri, hina na nardo,

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

13 Machipukizi yako ni bustani ya mikomamanga pamoja na matunda bora kuliko yote, hina na nardo.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

13 Machipukizi yako ni bustani ya mikomamanga pamoja na matunda bora kuliko yote, hina na nardo.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

13 Machipukizi yako ni bustani ya mikomamanga pamoja na matunda bora kuliko yote, hina na nardo.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

13 Mimea yako ni bustani ya mikomamanga yenye matunda mazuri sana, yenye hina na nardo,

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

13 Mimea yako ni bustani ya mikomamanga yenye matunda mazuri sana, yenye hina na nardo,

Tazama sura Nakili




Wimbo Ulio Bora 4:13
18 Marejeleo ya Msalaba  

Watazaa matunda hadi wakati wa uzee, Watajaa utomvu, watakuwa na ubichi.


nikajifanyia bustani na viunga, na kuipanda humo miti yenye matunda ya kila namna;


Muda mfalme alipoketi juu ya kochi, Nardo yangu ilitoa harufu yake.


Mpendwa wangu ni kama kishada cha hina, Katika mizabibu huko Engedi.


Kama mpera kati ya miti ya msituni, Kadhalika mpendwa wangu kati ya vijana. Niliketi kivulini mwake kwa furaha, Na matunda yake niliyaonja kuwa matamu.


Nardo na zafarani, mchai na mdalasini, Na miti yote iletayo ubani, Manemane na udi, na kolezi kuu zote.


Amka, kaskazi; nawe uje, kusi; Vumeni juu ya bustani yangu, Manukato ya bustani yatokee. Mpendwa wangu na aingie bustanini mwake, Akayale matunda yake mazuri.


Nilishukia katika bustani ya milozi, Ili kuyatazama machipuko ya bondeni; Nione kama mzabibu umechanua, Kama mikomamanga imetoa maua.


Mpendwa wangu ameshukia bustani yake, Kwenye matuta ya rihani; Ili kulisha penye bustani, Ili kuchuma nyinyoro.


Ningekuongoza nyumbani mwa mamangu, Naye angenifundisha; Ningekunywesha divai iliyokolea, Divai mpya ya mkomamanga wangu.


Watu wako nao watakuwa wenye haki wote, Nao watairithi nchi milele; Wao ni chipukizi nililolipanda mimi mwenyewe, Kazi ya mikono yangu mwenyewe, Ili mimi nitukuzwe.


Maana kama nchi itoavyo machipuko yake, na kama bustani ioteshavyo vitu vilivyopandwa ndani yake; ndivyo Bwana MUNGU atakavyootesha haki na sifa mbele ya mataifa yote.


Wala hapana mmoja amsukumaye mwenzake; huendelea mbele kila mmoja katika njia yake; hujifanyia njia kwa nguvu kati ya silaha, wala hawaachi kuifuata njia yao.


Naye alipokuwapo Bethania, nyumbani mwa Simoni mwenye ukoma, akiwa amekaa mezani, alikuja mwanamke mwenye chupa ya marhamu yenye manukato ya nardo safi ya thamani kubwa; akaivunja chupa akaimimina kichwani pake.


Basi Mariamu akatwaa ratili ya marhamu ya nardo safi yenye thamani nyingi, akampaka Yesu miguu, akamfuta miguu kwa nywele zake. Nayo nyumba pia ikajaa harufu ya marhamu.


akiwa mmejazwa matunda ya haki, kwa njia ya Yesu Kristo, kwa utukufu na sifa ya Mungu.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo