Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Waroma 7:15 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

15 Maana sijui nifanyalo, kwa sababu lile nilipendalo, silitendi; bali lile nilichukialo ndilo ninalolitenda.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

15 Sielewi nifanyacho, maana kile ninachotaka sikifanyi, bali kile ninachokichukia ndicho nikifanyacho.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

15 Sielewi nifanyacho, maana kile ninachotaka sikifanyi, bali kile ninachokichukia ndicho nikifanyacho.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

15 Sielewi nifanyacho, maana kile ninachotaka sikifanyi, bali kile ninachokichukia ndicho nikifanyacho.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

15 Sielewi nitendalo, kwa maana lile ninalotaka kulitenda, silitendi, lakini ninatenda lile ninalolichukia.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

15 Sielewi nitendalo, kwa maana lile ninalotaka kulitenda, silitendi, lakini ninatenda lile ninalolichukia.

Tazama sura Nakili




Waroma 7:15
32 Marejeleo ya Msalaba  

Ikiwa wamekutenda dhambi, (maana hakuna mtu asiyetenda dhambi), hata ukawaghadhibikia, ukawatia katika mikono ya adui zao, wawachukue mateka mpaka nchi ya adui zao, iliyo mbali au iliyo karibu;


Kwa kuwa BWANA anaijua njia ya wenye haki, Bali njia ya wasio haki itapotea.


Sitaweka mbele ya macho yangu Neno la uovu. Kazi yao waliopotoka naichukia, Haitaambatana nami.


Kwa mausia yako najipatia ufahamu, Ndiyo maana naichukia kila njia ya uongo.


Watu wa kusitasita nawachukia, Lakini sheria yako naipenda.


Maana nayafuata mausia yako yote, kuwa ya adili, Kila njia ya uongo naichukia.


Nimeuchukia uongo, umenikirihi, Sheria yako nimeipenda.


Nitakwenda mbio katika njia ya maagizo yako, Utakaponipanulia ufahamu wangu.


Tazama, nimeyatamani mausia yako, Unihuishe kwa haki yako.


Ni nani awezaye kuyatambua makosa yake? Unitakase na mambo ya siri.


Huwaza maovu kitandani pake, Hujiweka katika njia mbaya; hauchukii ubaya.


Tutakapozidiwa na matendo maovu Wewe utatuondolea uovu wetu.


Enyi mmpendao BWANA, uchukieni uovu; Huwalinda nafsi zao watauwa wake, Na kuwaokoa na mkono wa wasio haki.


Mwenye haki huchukia kusema uongo; Bali mtu mbaya huwa karaha, hupatwa na aibu.


Kumcha BWANA ni kuchukia uovu; Kiburi na majivuno, na njia mbovu, Na kinywa cha ukaidi pia nakichukia.


Bila shaka hakuna mwanadamu mwenye haki hapa duniani, atendaye mema pasipo kutenda dhambi.


Yachukieni mabaya; yapendeni mema; mkaithibitishe haki langoni; yamkini kwamba BWANA, Mungu wa majeshi, atawafanyia fadhili mabaki ya Yusufu.


BWANA ni mwema, ni ngome siku ya taabu; naye huwajua hao wamkimbiliao.


Basi, mwashuhudia na kuziridhia kazi za baba zenu; kwa kuwa wao waliwaua nanyi mwawajengea maziara.


Siwaiti tena watumwa; kwa maana mtumwa hajui atendalo bwana wake; lakini ninyi nimewaita rafiki; kwa kuwa yote niliyoyasikia kwa Baba yangu nimewaarifu.


Pendo na lisiwe na unafiki lichukieni lililo ovu, mkilishika lililo jema.


Ile imani uliyo nayo uwe nayo nafsini mwako mbele za Mungu. Heri mtu yule asiyejihukumu nafsi yake katika neno lile analolikubali.


Lakini kama nikilitenda lile nisilolipenda, naikiri ile sheria ya kuwa ni njema.


Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka.


Lakini msingi wa Mungu ulio imara umesimama, wenye mhuri huu, Bwana awajua walio wake. Na tena, Kila aliitaye jina la Bwana na auache uovu.


Umependa haki, umechukia maasi; Kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekutia mafuta, Mafuta ya shangwe kupita wenzio.


Maana twajikwaa sisi sote pia katika mambo mengi. Mtu asiyejikwaa katika kunena, huyo ni mtu mkamilifu, awezaye kuuzuia na mwili wake wote kama kwa lijamu.


na wengine waokoeni kwa kuwanyakua katika moto; na wengine wahurumieni kwa hofu, mkilichukia hata vazi lililotiwa uchafu na mwili.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo