Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Waroma 3:10 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

10 kama ilivyoandikwa, ya kwamba, Hakuna mwenye haki hata mmoja.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

10 Kama Maandiko Matakatifu yasemavyo: “Hakuna hata mmoja aliye mwadilifu!

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

10 Kama Maandiko Matakatifu yasemavyo: “Hakuna hata mmoja aliye mwadilifu!

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

10 Kama Maandiko Matakatifu yasemavyo: “Hakuna hata mmoja aliye mwadilifu!

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

10 Kama ilivyoandikwa: “Hakuna mwenye haki, hakuna hata mmoja.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

10 Kama ilivyoandikwa: “Hakuna mwenye haki, hakuna hata mmoja.

Tazama sura Nakili




Waroma 3:10
29 Marejeleo ya Msalaba  

Ni nani awezaye kutoa kitu kilicho safi kitoke katika kitu kichafu? Hapana awezaye.


Je! Mwanadamu ni kitu gani, hata akawa safi? Huyo aliyezaliwa na mwanamke, hata awe na haki?


Sembuse mtu ambaye ni mwenye kuchukiza na uchafu, Mwanadamu anywaye uovu kama anywavyo maji!


Basi mtu awezaje kuwa na haki mbele ya Mungu? Au awezaje kuwa safi aliyezaliwa na mwanamke?


Wala usimhukumu mtumishi wako, Maana kwako hakuna aliye hai mwenye haki.


Na waende kwa sheria na ushuhuda; ikiwa hawasemi kulingana na neno hili, bila shaka kwa hao hakuna asubuhi.


Moyo huwa mdanganyifu kuliko vitu vyote, una ugonjwa wa kufisha; nani awezaye kuujua?


Kwa maana moyoni hutoka mawazo mabaya, uuaji, uzinzi, uasherati; wizi, ushuhuda wa uongo, na matukano;


Yesu akamwambia, Kwa nini kuniita mwema? Hakuna aliye mwema ila mmoja, ndiye Mungu.


Kama ilivyoandikwa, Mungu aliwapa roho ya usingizi, macho hata wasione, na masikio hata wasisikie, hata siku hii ya leo.


Hakuna afahamuye; Hakuna amtafutaye Mungu.


kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu;


La hasha! Mungu aonekane kuwa kweli japo kila mtu ni mwongo; kama ilivyoandikwa, Ili ujulikane kuwa una haki katika maneno yako, Ukashinde uingiapo katika hukumu.


Maana hapo zamani sisi nasi tulikuwa hatuna akili, tulikuwa waasi, tumedanganywa, huku tukitumikia tamaa na anasa za namna nyingi, tukiishi katika uovu na husuda, tukichukiza na kuchukiana.


kwa maana imeandikwa, Mtakuwa watakatifu kwa kuwa mimi ni mtakatifu.


Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili.


Huko nje wako mbwa, na wachawi, na wazinzi, na wauaji, na hao waabuduo sanamu, na kila mtu apendaye uongo na kuufanya.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo