Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Waroma 12:15 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

15 Furahini pamoja nao wafurahio; lieni pamoja nao waliao.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

15 Furahini pamoja na wenye kufurahi, lieni pamoja na wenye kulia.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

15 Furahini pamoja na wenye kufurahi, lieni pamoja na wenye kulia.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

15 Furahini pamoja na wenye kufurahi, lieni pamoja na wenye kulia.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

15 Furahini pamoja na wenye kufurahi, lieni pamoja na wale waliao.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

15 Furahini pamoja na wenye kufurahi, lieni pamoja na wale waliao.

Tazama sura Nakili




Waroma 12:15
20 Marejeleo ya Msalaba  

Hapo niliposikia maneno hayo, nikaketi, nikalia, nikaomboleza siku kadhaa; kisha nikafunga, nikaomba mbele za Mungu wa mbinguni;


Basi ikawa hao marafiki watatu wa Ayubu walipopata habari ya mabaya hayo yote yaliyomfikia, wakaja kila mtu kutoka mahali pake; nao ni Elifazi Mtemani, na Bildadi Mshuhi, na Sofari Mnaamathi; wakapatana pamoja ili waende kumfariji Ayubu na kumtuliza moyo.


Je! Mimi sikulia kwa ajili ya huyo aliyekuwa katika taabu? Nafsi yangu, je! Haikusononeka kwa ajili ya wahitaji?


Wakati wa kulia, na wakati wa kucheka; Wakati wa kuomboleza, na wakati wa kucheza;


Naye Ebedmeleki, Mkushi, akamwambia Yeremia, Tia nguo hizi zilizotupwa, na vitambaa hivi vikuukuu, chini ya kamba kwapani. Naye Yeremia akafanya hivyo.


Laiti kichwa changu kingekuwa maji, na macho yangu kuwa chemchemi ya machozi, ili nipate kulia mchana na usiku kwa ajili yao waliouawa wa binti ya watu wangu!


Wakasikia jirani zake na jamaa zake ya kwamba Bwana amemwongezea rehema zake, wakafurahi pamoja naye.


na watu wengi katika Wayahudi walikuwa wamekuja kwa Martha na Mariamu, ili kuwafariji kwa ajili ya ndugu yao.


Naye, alipofika na kuiona neema ya Mungu akafurahi, akawasihi wote waambatane na Bwana kwa moyo wote.


Na kiungo kimoja kikiumia, viungo vyote huumia nacho, na kiungo kimoja kikitukuzwa, viungo vyote hufurahi pamoja nacho.


Ni nani aliye dhaifu, nisiwe dhaifu nami? Ni nani aliyekwazwa nami nisichukiwe?


Nami niliwaandikia neno lilo hilo, ili nijapo nisitiwe huzuni na wale ambao ilinipasa kuwafurahia; nikiwatumaini ninyi nyote kwamba furaha yangu ni yenu nyote pia.


Kwa kuwa alikuwa na shauku kwenu ninyi nyote, akahuzunika sana, kwa sababu mlisikia ya kwamba alikuwa mgonjwa.


Kwa hiyo nimefanya bidii nyingi zaidi kumtuma, ili mtakapomwona tena mpate kufurahi, nami nipunguziwe huzuni yangu.


Wakumbukeni hao waliofungwa kana kwamba mmefungwa pamoja nao; na hao wanaodhulumiwa, kwa vile ninyi nanyi mlivyo katika mwili.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo