Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Wakolosai 3:20 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

20 Ninyi watoto, watiini wazazi wenu katika mambo yote; maana jambo hili lapendeza katika Bwana.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

20 Enyi watoto, watiini wazazi wenu daima maana hiyo humpendeza Bwana.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

20 Enyi watoto, watiini wazazi wenu daima maana hiyo humpendeza Bwana.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

20 Enyi watoto, watiini wazazi wenu daima maana hiyo humpendeza Bwana.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

20 Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika mambo yote, kwa maana hii inampendeza Bwana Isa.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

20 Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika mambo yote, kwa maana hivi ndivyo inavyompendeza Bwana Isa.

Tazama sura Nakili




Wakolosai 3:20
23 Marejeleo ya Msalaba  

na ya kuwa Yakobo amewatii babaye na mamaye, akaenda Padan-aramu.


Waheshimu baba yako na mama yako; siku zako zipate kuwa nyingi katika nchi upewayo na BWANA, Mungu wako.


Amlaaniye babaye au mamaye, Taa yake itazimika katika giza kuu.


Kuna kizazi cha watu wamlaanio baba yao; Wala hawambariki mama yao.


Jicho la mtu amdhihakiye babaye, Na kudharau kumtii mamaye; Kunguru wa bondeni wataling'oa, Na vifaranga vya tai watalila.


Mwanangu, shika maagizo ya baba yako, Wala usiiache sheria ya mama yako.


Nasi tumeitii sauti ya Yonadabu, mwana wa Rekabu, baba yetu, katika yote aliyotuamuru, kwamba tusinywe divai siku zetu zote, sisi, na wake zetu, na wana wetu, na binti zetu;


Ndani yako wamedharau baba na mama; kati yako wamewatenda wageni udhalimu; ndani yako wamewaonea yatima na mjane.


Kila mtu na amche mama yake, na baba yake, nanyi mtazitunza Sabato zangu; mimi ndimi BWANA, Mungu wenu.


Mwana humheshimu baba yake, na mtumishi humcha bwana wake; basi, kama mimi ni baba yenu, heshima yangu iko wapi? Na kama mimi ni bwana wenu, kicho changu ki wapi? BWANA wa majeshi awauliza ninyi, enyi makuhani, mnaolidharau jina langu. Nanyi mwasema, Tumelidharau jina lako kwa jinsi gani?


Waheshimu baba yako na mama yako, na, Mpende jirani yako kama nafsi yako.


Lakini kama vile kanisa limtiivyo Kristo vivyo hivyo wake nao wawatii waume zao katika kila jambo.


Na alaaniwe amdharauye baba yake au mama yake. Na watu wote waseme, Amina.


Waheshimu baba yako na mama yako; kama BWANA, Mungu wako, alivyokuamuru, siku zako zipate kuzidi, nawe upate kufanikiwa katika nchi upewayo na BWANA, Mungu wako.


Lakini ninavyo vitu vyote na kuzidi, tena nimejaa tele; nimepokea kwa mkono wa Epafrodito vitu vile vilivyotoka kwenu, harufu ya manukato, sadaka yenye kibali, impendezayo Mungu.


mwenende kama ulivyo wajibu wenu kwa Bwana, mkimpendeza kabisa; mkizaa matunda kwa kila kazi njema, na kuzidi katika maarifa ya Mungu;


Ninyi watumwa, watiini hao ambao kwa mwili ni bwana zenu, katika mambo yote, si kwa utumwa wa macho, kama wajipendekezao kwa wanadamu, bali kwa unyofu wa moyo, mkimcha Bwana.


Watumwa na wawatii bwana zao, wakiwapendeza katika mambo yote; wasiwe wakaidi,


awafanye ninyi kuwa wakamilifu katika kila tendo jema, mpate kuyafanya mapenzi yake, naye akifanya ndani yetu lipendezalo mbele zake, kwa Yesu Kristo; utukufu una yeye milele na milele. Amina.


Akamwambia, Hayo yote unenayo mimi nitayafanya.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo