Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Wakolosai 2:9 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

9 Maana katika yeye unakaa utimilifu wote wa Mungu, kwa jinsi ya kimwili.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

9 Maana, ndani yake Kristo katika ubinadamu wake, umo ukamilifu wote wa Mungu,

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

9 Maana, ndani yake Kristo katika ubinadamu wake, umo ukamilifu wote wa Mungu,

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

9 Maana, ndani yake Kristo katika ubinadamu wake, umo ukamilifu wote wa Mungu,

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

9 Maana utimilifu wote wa Mungu unakaa ndani ya Al-Masihi katika umbile la mwili wa kibinadamu,

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

9 Maana ukamilifu wote wa Uungu umo ndani ya Al-Masihi katika umbile la mwili wa kibinadamu,

Tazama sura Nakili




Wakolosai 2:9
20 Marejeleo ya Msalaba  

Kwa hiyo Bwana mwenyewe atawapa ishara. Tazama, bikira atachukua mimba, atazaa mtoto wa kiume, naye atamwita jina lake Imanueli.


Tazama, bikira atachukua mimba, Naye atazaa mwana; Nao watamwita jina lake Imanueli; Yaani, Mungu pamoja nasi.


Mtumwa akasema, Bwana, hayo uliyoagiza yamekwisha tendeka, na hata sasa ingaliko nafasi.


Roho Mtakatifu akashuka juu yake kwa mfano wa kiwiliwili, kama hua; sauti ikatoka mbinguni, Wewe ndiwe Mwanangu, mpendwa wangu; nimependezwa nawe.


Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu; nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba; amejaa neema na kweli.


Kwa kuwa katika utimilifu wake sisi sote tulipokea, na neema juu ya neema.


Mimi na Baba tu mmoja.


lakini nikizitenda, ijapokuwa hamniamini mimi, ziaminini zile kazi; mpate kujua na kufahamu ya kuwa Baba yu ndani yangu, nami ni ndani ya Baba.


Siku ile ninyi mtatambua ya kuwa mimi ni ndani ya Baba yangu, nanyi ndani yangu, nami ndani yenu.


Wote wawe na umoja; kama wewe, Baba, ulivyo ndani yangu, nami ndani yako; hao nao wawe ndani yetu; ili ulimwengu upate kusadiki ya kwamba wewe ndiwe uliyenituma.


Lakini yeye alinena habari za hekalu la mwili wake.


Basi, kwa kuwa sisi tu wazawa wa Mungu, haitupasi kudhani ya kuwa Uungu ni mfano wa dhahabu au fedha au jiwe, vitu vilivyochongwa kwa ustadi na akili za wanadamu.


yaani, Mungu alikuwa ndani ya Kristo, akiupatanisha ulimwengu na nafsi yake, asiwahesabie makosa yao; naye ametia ndani yetu neno la upatanisho.


Kwa kuwa katika yeye ilipendeza utimilifu wote ukae;


Na bila shaka siri ya utauwa ni kuu. Mungu alidhihirishwa katika mwili, Akajulikana kuwa na haki katika roho, Akaonekana na malaika, Akahubiriwa katika mataifa, Akaaminiwa katika ulimwengu, Akachukuliwa juu katika utukufu.


tukilitazamia tumaini lenye baraka na kufunuliwa kwa utukufu wa Kristo Yesu, Mungu mkuu na Mwokozi wetu;


Nasi tunajua kwamba Mwana wa Mungu amekwisha kuja, naye ametupa akili kwamba tumjue yeye aliye wa kweli, nasi tumo ndani yake yeye aliye wa kweli, yaani, ndani ya Mwana wake Yesu Kristo. Huyu ndiye Mungu wa kweli, na uzima wa milele.


Naye Roho ndiye ashuhudiaye, kwa sababu Roho ndiye kweli.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo