Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Waefeso 3:14 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

14 Kwa hiyo nampigia Baba magoti,

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

14 Kwa sababu hiyo, nampigia magoti Baba,

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

14 Kwa sababu hiyo, nampigia magoti Baba,

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

14 Kwa sababu hiyo, nampigia magoti Baba,

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

14 Kwa sababu hii nampigia Baba magoti,

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

14 Kwa sababu hii nampigia Baba magoti,

Tazama sura Nakili




Waefeso 3:14
16 Marejeleo ya Msalaba  

Pamoja na hayo nitajisazia katika Israeli watu elfu saba, kila goti lisilomwinamia Baali, na kila kinywa kisichombusu.


Hata ikawa, Sulemani alipokwisha kumwomba BWANA maombi hayo, na dua hiyo yote, akasimama na kuondoka hapo mbele ya madhabahu ya BWANA, hapo alipokuwa amepiga magoti, na kuikunjua mikono yake kuelekea mbinguni.


(maana Sulemani alikuwa amefanya mimbari ya shaba, urefu wake dhiraa tano, na upana wake dhiraa tano, na kwenda juu kwake dhiraa tatu, na kuisimamisha katikati ya ua; akasimama juu yake, akapiga magoti mbele ya mkutano wote wa Israeli, akaikunjua mikono yake kuelekea mbinguni);


Na wakati wa sadaka ya jioni nikainuka baada ya kunyenyekea kwangu, nguo yangu na joho langu zimeraruliwa, nikaanguka magotini nikakunjua mikono yangu mbele za BWANA, Mungu wangu;


Njoni, tuabudu, tusujudu, Tupige magoti mbele za BWANA aliyetuumba.


Kwa nafsi yangu nimeapa, neno hili limetoka kinywani mwangu katika haki, wala halitarudi, ya kwamba mbele zangu kila goti litapigwa, kila ulimi utaapa.


Hata Danieli, alipojua ya kuwa yale maandiko yamekwisha kutiwa sahihi, akaingia nyumbani mwake, (na madirisha katika chumba chake yalikuwa yamefunguliwa kuelekea Yerusalemu;) akapiga magoti mara tatu kila siku, akasali, akashukuru mbele za Mungu wake, kama alivyokuwa akifanya tokea hapo.


Mwenyewe akajitenga nao kama kiasi cha kutupa jiwe, akapiga magoti akaomba,


Alipokwisha kunena haya akapiga magoti, akaomba pamoja nao wote.


Hata tulipotimiza siku zile tukaondoka tukaenda zetu, na watu wote, pamoja na wake zao na watoto wao, wakatusindikiza mpake nje ya mji, tukapiga magoti pwani tukaomba;


Akapiga magoti, akalia kwa sauti kuu, Bwana, usiwahesabie dhambi hii. Akiisha kusema haya akalala. Na Sauli alikuwa akiona kitendo cha kuuawa kwake kuwa sawa.


Petro akawatoa nje wote, akapiga magoti, akaomba, kisha akaelekea yule maiti, akanena, Tabitha, inuka. Naye akafumbua macho yake, na alipomwona Petro akajiinua, akaketi.


Atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, aliyetubariki kwa baraka zote za rohoni, katika ulimwengu wa roho, ndani yake Kristo;


ambaye kwa jina lake ubaba wote wa mbinguni na wa duniani unaitwa,


ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi;


Tufuate:

Matangazo


Matangazo