Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Waamuzi 13:23 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

23 Lakini mkewe akamwambia, Kama BWANA angetaka kutuua hangepokea sadaka ya kuteketezwa, wala sadaka ya unga, mikononi mwetu, wala hangetuonesha mambo hayo yote, wala hangetuambia mambo kama hayo wakati huu.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

23 Lakini mkewe akamjibu, “Kama Mwenyezi-Mungu angetaka kutuua hangepokea sadaka yetu ya kuteketezwa na ya nafaka; wala hangetuonesha mambo hayo wala kutuambia maagizo.”

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

23 Lakini mkewe akamjibu, “Kama Mwenyezi-Mungu angetaka kutuua hangepokea sadaka yetu ya kuteketezwa na ya nafaka; wala hangetuonesha mambo hayo wala kutuambia maagizo.”

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

23 Lakini mkewe akamjibu, “Kama Mwenyezi-Mungu angetaka kutuua hangepokea sadaka yetu ya kuteketezwa na ya nafaka; wala hangetuonesha mambo hayo wala kutuambia maagizo.”

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

23 Lakini mkewe akamwambia, “Ikiwa Mwenyezi Mungu alikuwa amekusudia kutuua, hangepokea sadaka ya kuteketezwa na sadaka ya unga kutoka mikononi mwetu, wala hangetuonesha mambo haya yote wala kututangazia mambo haya wakati huu.”

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

23 Lakini mkewe akamwambia, “Ikiwa bwana alikuwa amekusudia kutuua, asingelipokea sadaka ya kuteketezwa na sadaka ya unga kutoka mikononi mwetu, wala asingelituonyesha mambo haya yote wala kututangazia mambo kama haya wakati huu.”

Tazama sura Nakili




Waamuzi 13:23
12 Marejeleo ya Msalaba  

Akujalie kwa kadiri ya haja ya moyo wako, Na kukutimizia mipango yako yote.


Siri ya BWANA iko kwao wamchao, Naye atawajulisha agano lake.


Naamini ya kuwa nitauona wema wa BWANA Katika nchi ya walio hai.


Unifanyie ishara ya wema, Wanichukiao waione na kuaibishwa. Kwa kuwa Wewe, BWANA, Umenisaidia na kunifariji.


Maana mtu mjeuri ni chukizo kwa BWANA, Bali siri yake ni pamoja na wanyofu.


Siku ile ninyi mtatambua ya kuwa mimi ni ndani ya Baba yangu, nanyi ndani yangu, nami ndani yenu.


Yesu akajibu, akamwambia, Mtu akinipenda, atalishika neno langu; na Baba yangu atampenda; nasi tutakuja kwake, na kufanya makao kwake.


Siwaiti tena watumwa; kwa maana mtumwa hajui atendalo bwana wake; lakini ninyi nimewaita rafiki; kwa kuwa yote niliyoyasikia kwa Baba yangu nimewaarifu.


Na jicho haliwezi kuuambia mkono, Sina haja na wewe; wala tena kichwa hakiwezi kuiambia miguu, Sina haja na ninyi.


Basi yule mwanamke akamzaa mtoto wa kiume akamwita jina lake Samsoni, mtoto huyu akakua, BWANA akambariki.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo