Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Ufunuo 7:16 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

16 Hawataona njaa tena, wala hawataona kiu tena, wala jua halitawapiga, wala joto iliyo yote.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

16 Hawataona tena njaa wala kiu; jua wala joto kali halitawachoma tena,

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

16 Hawataona tena njaa wala kiu; jua wala joto kali halitawachoma tena,

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

16 Hawataona tena njaa wala kiu; jua wala joto kali halitawachoma tena,

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

16 Kamwe hawataona njaa wala kiu tena. Jua halitawachoma wala joto lolote liunguzalo.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

16 Kamwe hawataona njaa wala kiu tena. Jua halitawapiga wala joto lolote liunguzalo.

Tazama sura Nakili




Ufunuo 7:16
23 Marejeleo ya Msalaba  

BWANA ndiye mlinzi wako; BWANA ni uvuli katika mkono wako wa kulia.


Jua halitakupiga mchana, Wala mwezi wakati wa usiku.


Nakunyoshea mikono yangu; Nafsi yangu inakuonea kiu kama nchi kame.


Nafsi yangu inamwonea kiu MUNGU, Mungu aliye hai, Lini nitakapokuja nionekane mbele za Mungu?


Ee MUNGU, Mungu wangu, nitakutafuta mapema, Nafsi yangu inakuonea kiu, Mwili wangu wakuonea shauku, Katika nchi kame na uchovu, isiyo na maji.


Msinichunguze kwa kuwa ni mweusi mweusi, Kwa sababu jua limeniunguza. Wana wa mamangu walinikasirikia, Waliniweka niwe mlinzi wa mashamba ya mizabibu; Bali shamba langu mwenyewe sikulilinda.


Maana umekuwa ngome ya maskini, Ngome ya mhitaji katika dhiki yake, Mahali pa kukimbilia wakati wa tufani, Na kivuli wakati wa joto; Wakati kishindo cha watu wakatili kilipokuwa, Kama dhoruba ipigayo ukuta.


Na mwanadamu atakuwa kama mahali pa kujificha na upepo, na mahali pa kujisitiri na dhoruba; kama mito ya maji mahali pakavu, kama kivuli cha mwamba mkubwa katika nchi yenye uchovu.


Maskini na wahitaji wanatafuta maji, wala hapana; ndimi zao zimekauka kwa kiu; mimi, BWANA, nitawasikia, mimi, Mungu wa Israeli, sitawaacha.


Hawataona njaa, wala hawataona kiu; joto halitawapiga, wala jua; kwa maana yeye aliyewarehemu atawatangulia, naam, karibu na chemchemi za maji atawaongoza.


Kwa hiyo Bwana MUNGU asema hivi, Tazama, watumishi wangu watakula, bali ninyi mtaona njaa; tazama, watumishi wangu watakunywa, bali ninyi mtaona kiu; tazama, watumishi wangu watafurahi, bali ninyi mtatahayarika;


Basi ikawa, jua lilipopanda juu, Mungu akatayarisha upepo wa mashariki, wenye joto jingi; jua likampiga Yona kichwani, hata akazimia, naye akajitakia kufa, akasema, Ni afadhali nife mimi kuliko kuishi.


lakini hana mizizi ndani yake, bali hudumu kwa muda; ikitukia dhiki au udhia kwa ajili ya lile neno, mara huchukizwa.


Lakini jua lilipozuka ziliungua; na kwa kuwa hazina mizizi zikanyauka.


Heri wenye njaa na kiu ya haki; Maana hao watashibishwa.


ila hawana mizizi ndani yao, bali hudumu muda mchache; kisha ikitokea dhiki au udhia kwa ajili ya lile neno, mara hujikwaa.


hata jua lilipozuka iliungua, na kwa kuwa haina mizizi ikanyauka.


Wenye njaa amewashibisha mema, Na wenye mali amewaondoa mikono mitupu.


Heri ninyi mlio na njaa sasa, kwa sababu mtashiba. Heri ninyi mliao sasa, kwa sababu mtacheka.


lakini yeyote atakayekunywa maji yale nitakayompa mimi hataona kiu milele; bali yale maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji, yakibubujikia uzima wa milele.


Maana jua huchomoza kwa joto kali, huyakausha majani; ua lake huanguka, uzuri wa umbo lake hupotea; vivyo hivyo naye tajiri atanyauka katika njia zake.


Naye atafuta kila chozi katika macho yao, wala mauti haitakuwapo tena; wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu hayatakuwapo tena; kwa kuwa mambo ya kwanza yamekwisha kupita.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo