Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Ufunuo 18:7 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

7 Kwa kadiri alivyojitukuza na kufanya anasa, mpeni maumivu na huzuni kadiri iyo hiyo. Kwa kuwa husema moyoni mwake, Nimeketi malkia, wala si mjane, wala sitaona huzuni kamwe.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

7 Mpeni mateso na uchungu kadiri ya kujigamba kwake, kulingana na kuishi kwake kwa anasa. Maana anajisemea moyoni: ‘Ninaketi hapa; mimi ni malkia. Mimi si mjane, wala sitapatwa na uchungu!’

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

7 Mpeni mateso na uchungu kadiri ya kujigamba kwake, kulingana na kuishi kwake kwa anasa. Maana anajisemea moyoni: ‘Ninaketi hapa; mimi ni malkia. Mimi si mjane, wala sitapatwa na uchungu!’

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

7 Mpeni mateso na uchungu kadiri ya kujigamba kwake, kulingana na kuishi kwake kwa anasa. Maana anajisemea moyoni: ‘Ninaketi hapa; mimi ni malkia. Mimi si mjane, wala sitapatwa na uchungu!’

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

7 Mpatie mateso na huzuni nyingi sawa na utukufu na anasa alizojipatia. Kwa kuwa moyoni mwake hujivuna, akisema, ‘Mimi ninatawala kama malkia; mimi si mjane, wala sitaona huzuni kamwe.’

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

7 Mpatie mateso na huzuni nyingi sawa na utukufu na anasa alizojipatia. Kwa kuwa moyoni mwake hujivuna, akisema, ‘Mimi ninatawala kama malkia; mimi si mjane, wala sitaona huzuni kamwe.’

Tazama sura Nakili




Ufunuo 18:7
16 Marejeleo ya Msalaba  

Basi mfalme akamwambia Hamani, Hima! Twaa mavazi na farasi kama ulivyosema, ukamfanyie vivyo hivyo Mordekai, Myahudi, aketiye mlangoni pa mfalme; lisipungue neno lolote katika yote uliyoyasema.


Asema moyoni mwake, Sitaondoshwa, Kizazi baada ya kizazi sitakuwamo taabuni.


Binti za wafalme wamo Miongoni mwa akina bibi wako wastahiki. Katika mkono wako wa kulia amesimama malkia Akiwa amevaa dhahabu safi ya Ofiri.


Mwambie mfalme, na mama ya mfalme, Nyenyekeeni na kuketi chini; Kwa maana vilemba vyenu vimeshuka, naam, taji la utukufu wenu.


Jinsi mji huu ukaavyo ukiwa, Huo uliokuwa umejaa watu! Jinsi alivyokuwa kama mjane, Yeye aliyekuwa mkuu kati ya mataifa! Binti mfalme kati ya majimbo, Jinsi alivyoshikwa shokoa!


Naam, utakinywea hata hakitabaki kitu ndani yake, utavitafuna vigae vyake, utayararua maziwa yako; maana mimi, Bwana MUNGU, nimenena neno hili.


Kiburi cha moyo wako kimekudanganya, Wewe ukaaye katika pango za majabali, Mwenye makao yako juu sana; Asemaye moyoni, Ni nani atakayenishusha mimi?


Huu ndio mji ule wa furaha, Uliokaa salama, Uliosema moyoni mwake, Mimi niko, Wala hapana mwingine ila mimi. Jinsi ulivyokuwa ukiwa, Mahali pa kulala pa wanyama wa bara! Kila mtu apitaye atazomea, Na kutikisa mkono wake.


Bali wajane walio vijana ukatae kuwaandika hao, maana, wakizidiwa na tamaa kinyume cha Kristo, wataka kuolewa;


kwa kuwa mataifa yote wamekunywa mvinyo ya ghadhabu ya uasherati wake, na wafalme wa nchi wamezini naye, na wafanya biashara wa nchi wamepata mali kwa nguvu za kiburi chake.


Na hao wafalme wa nchi, waliozini naye na kufanya anasa pamoja naye, watalia na kumwombolezea; wauonapo moshi wa kuungua kwake;


Tufuate:

Matangazo


Matangazo