Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Kitabu hiki si kilichoandikwa kwa uvuvio wa Mungu, na si sehemu ya kanoni ya Kikristo wala Tanaki ya Kiyahudi. Kinaonyeshwa kwa madhumuni ya kihistoria na ya utafiti tu. Tazama maelezo kamili

Tobiti 10:12 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

12 Akamwambia binti yake, Waheshimu wakwezo, walio sasa kama wazazi wako; ili nipate sifa zako njema. Akambusu. Edna naye akamwambia Tobia, Ndugu yangu mpenzi, Mungu wa mbinguni akurudishe, na anijalie kuwaona watoto wako atakaokuzalia binti yangu Sara, ili nifurahi mbele za BWANA. Angalia, nimekukabidhi binti yangu amana bora, maana usimchokoze.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

12 Kisha akambusu binti yake Sara na kusema, “Nenda sasa nyumbani kwa baba mkwe wako, kwani tangu sasa wazazi wa mumeo ni wazazi wako kama sisi tulivyo wazazi wako. Nenda kwa amani, binti yangu. Natumaini kusikia mema juu yako kadiri niishivyo.” Kisha akawaaga na kuwaacha waende zao. Naye Edna akamwambia Tobia, “Mwanangu mpendwa na ndugu Tobia, Bwana wa mbinguni akurudishe tena salama! Nami natumaini kuishi hata niwaone watoto wako na binti yangu Sara kabla sijafa. Mbele ya Bwana namkabidhi binti yangu mikononi mwako. Kamwe usimhuzunishe maishani mwako. Nenda kwa amani mwanangu. Tangu sasa mimi ni mama yako na Sara ni dada yako mpendwa. Na sote tuishi kwa amani siku zote za maisha yetu!” Basi akawabusu wote wawili na kuwaacha kwa furaha.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

12 Kisha akambusu binti yake Sara na kusema, “Nenda sasa nyumbani kwa baba mkwe wako, kwani tangu sasa wazazi wa mumeo ni wazazi wako kama sisi tulivyo wazazi wako. Nenda kwa amani, binti yangu. Natumaini kusikia mema juu yako kadiri niishivyo.” Kisha akawaaga na kuwaacha waende zao. Naye Edna akamwambia Tobia, “Mwanangu mpendwa na ndugu Tobia, Bwana wa mbinguni akurudishe tena salama! Nami natumaini kuishi hata niwaone watoto wako na binti yangu Sara kabla sijafa. Mbele ya Bwana namkabidhi binti yangu mikononi mwako. Kamwe usimhuzunishe maishani mwako. Nenda kwa amani mwanangu. Tangu sasa mimi ni mama yako na Sara ni dada yako mpendwa. Na sote tuishi kwa amani siku zote za maisha yetu!” Basi akawabusu wote wawili na kuwaacha kwa furaha.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

12 Akamwambia binti yake, Waheshimu wakwezo, walio sasa kama wazazi wako; ili nipate sifa zako njema. Akambusu. Edna naye akamwambia Tobia, Ndugu yangu mpenzi, Mungu wa mbinguni akurudishe, na anijalie kuwaona watoto wako atakaokuzalia binti yangu Sara, ili nifurahi mbele za BWANA. Angalia, nimekukabidhi binti yangu amana bora, kwa hiyo usimchokoze.

Tazama sura Nakili

BIBLIA Yenye Vitabu vya Deuterokanoni HABARI NJEMA

12 Kisha akambusu binti yake Sara na kusema, “Nenda sasa nyumbani kwa baba mkwe wako, kwani tangu sasa wazazi wa mumeo ni wazazi wako kama sisi tulivyo wazazi wako. Nenda kwa amani, binti yangu. Natumaini kusikia mema juu yako kadiri niishivyo.” Kisha akawaaga na kuwaacha waende zao. Naye Edna akamwambia Tobia, “Mwanangu mpendwa na ndugu Tobia, Bwana wa mbinguni akurudishe tena salama! Nami natumaini kuishi hata niwaone watoto wako na binti yangu Sara kabla sijafa. Mbele ya Bwana namkabidhi binti yangu mikononi mwako. Kamwe usimhuzunishe maishani mwako. Nenda kwa amani mwanangu. Tangu sasa mimi ni mama yako na Sara ni dada yako mpendwa. Na sote tuishi kwa amani siku zote za maisha yetu!” Basi akawabusu wote wawili na kuwaacha kwa furaha.

Tazama sura Nakili




Tobiti 10:12
0 Marejeleo ya Msalaba  

Tufuate:

Matangazo


Matangazo