Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Mhubiri 7:20 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

20 Bila shaka hakuna mwanadamu mwenye haki hapa duniani, atendaye mema pasipo kutenda dhambi.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

20 Hakika, hakuna mtu mwadilifu duniani atendaye mema daima bila kutenda dhambi.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

20 Hakika, hakuna mtu mwadilifu duniani atendaye mema daima bila kutenda dhambi.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

20 Hakika, hakuna mtu mwadilifu duniani atendaye mema daima bila kutenda dhambi.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

20 Hakuna mtu mwenye haki duniani ambaye hufanya mambo ya haki na kamwe asitende dhambi.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

20 Hakuna mtu mwenye haki duniani ambaye hufanya mambo ya haki na kamwe asitende dhambi.

Tazama sura Nakili




Mhubiri 7:20
16 Marejeleo ya Msalaba  

Ikiwa wamekutenda dhambi, (maana hakuna mtu asiyetenda dhambi), hata ukawaghadhibikia, ukawatia katika mikono ya adui zao, wawachukue mateka mpaka nchi ya adui zao, iliyo mbali au iliyo karibu;


Wakikukosa, (maana hakuna mtu asiyekosa), hata uwakasirikie, na kuwatia mikononi mwa adui zao, wawahamishe, na kuwachukua mateka mpaka nchi iliyo mbali au iliyo karibu;


Tazama, nitakujibu, katika neno hili huna haki; Kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mwanadamu.


BWANA, kama Wewe ungehesabu maovu, Ee Bwana, nani angesimama?


Mpumbavu husema moyoni, Hakuna Mungu; Wameharibu matendo yao na kuyafanya chukizo, Hakuna atendaye mema.


Wote wamepotoka, wameoza wote pamoja, Hakuna atendaye mema, La! Hata mmoja.


Wala usimhukumu mtumishi wako, Maana kwako hakuna aliye hai mwenye haki.


Nani awezaye kusema, Nimesafisha moyo wangu; Nimetakasika dhambi yangu?


Sisi sote kama kondoo tumepotea; Kila mmoja wetu amegeukia njia yake mwenyewe; Na BWANA ameweka juu yake Maovu yetu sisi sote.


Kwa maana sisi sote tumekuwa kama mtu aliye mchafu, na matendo yetu yote ya haki yamekuwa kama nguo iliyotiwa unajisi; sisi sote twanyauka kama jani, na maovu yetu yatuondoa, kama upepo uondoavyo.


ndipo kuhani ataangalia; ikiwa vile vipaku ving'aavyo vilivyo katika ngozi ya mwili wake ni vyeupe kidogo; ni mba iliyotokeza katika ngozi; yeye ni safi.


kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu;


Maana twajikwaa sisi sote pia katika mambo mengi. Mtu asiyejikwaa katika kunena, huyo ni mtu mkamilifu, awezaye kuuzuia na mwili wake wote kama kwa lijamu.


Basi Yonathani akaondoka pale mezani, akiwa na hasira kali, wala hakula chakula siku ya pili ya mwezi, kwa sababu alimhuzunikia Daudi sana, na kwa sababu baba yake amemwaibisha.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo