Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Mhubiri 5:17 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

17 Siku zake zote hula gizani, mwenye fadhaa nyingi, mwenye ugonjwa na uchungu.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

17 Aliishi maisha yake yote katika giza na huzuni; katika mahangaiko, magonjwa na hasira.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

17 Aliishi maisha yake yote katika giza na huzuni; katika mahangaiko, magonjwa na hasira.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

17 Aliishi maisha yake yote katika giza na huzuni; katika mahangaiko, magonjwa na hasira.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

17 Siku zake zote hula gizani, pamoja na fadhaa kubwa, mateso na hasira.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

17 Siku zake zote hula gizani, pamoja na fadhaa kubwa, mateso na hasira.

Tazama sura Nakili




Mhubiri 5:17
21 Marejeleo ya Msalaba  

Akamwambia Adamu, Kwa kuwa umeisikiliza sauti ya mke wako, ukala matunda ya mti ambao nilikuagiza, nikisema, Usiyale; ardhi imelaaniwa kwa ajili yako; kwa uchungu utakula mazao yake siku zote za maisha yako;


Naye akasema, Kama BWANA, Mungu wako, aishivyo, sina mkate, ila konzi ya unga katika pipa, na mafuta kidogo katika chupa; nami ninaokota kuni mbili ili niingie nijipikie mwenyewe na mwanangu, tule kisha tufe.


Na Ahazia akaanguka kutoka dirisha la chumba chake ghorofani, katika Samaria, akaugua; akatuma wajumbe, akawaambia, Nendeni mkaulize kwa Baal-zebubu, mungu wa Ekroni, kama nitapona ugonjwa huu.


Wakamwambia, Mtu alitokea, akaonana nasi, akatuambia, Nendeni, rudini kwa mfalme yule aliyewatuma, mkamwambie, BWANA asema hivi Je! Ni kwa sababu hapana Mungu katika Israeli, hata mnakwenda kuuliza kwa Baal-zebubu, mungu wa Ekroni? Basi kwa ajili ya hayo hutashuka katika kile kitanda ulichokipanda, bali hakika utakufa.


Basi ukoma wa Naamani utakushika wewe, na wazao wako hata milele. Naye akatoka usoni pake mwenye ukoma kama theluji.


Mwingine hufa katika uchungu wa roho, Asionje mema kamwe.


Maana ninakula majivu kama chakula, Na kukichanganya kinywaji changu na machozi.


Kazi yenu ni bure, mnaoamka mapema, Na kukawia kwenda kulala, Na kula chakula cha taabu; Yeye humpa mpenzi wake usingizi.


Kweli, watu wote hupita kama kivuli; Wao hujisumbua bure tu; Wanajirundikia mali wala hawajui ni nani atakayeirithi.


Kwa hiyo akazikomesha siku zao kama pumzi, Na miaka yao kwa hofu ya kuwastusha.


Wala sikuyanyima macho yangu chochote yalichokitamani; wala sikuuzuia moyo wangu katika furaha yoyote; maana moyo wangu ulifurahi kwa sababu ya kazi yangu yote, na hii ilikuwa sehemu yangu katika kazi yangu yote.


Kwa kuwa siku zake zote ni masikitiko, na kazi yake ni huzuni; naam, hata usiku moyoni mwake hamna raha. Hayo nayo ni ubatili.


Mwanadamu hapati jema kupita kula na kunywa, na kuiburudisha roho yake kwa mema katika kazi yake. Hayo nayo niliona ya kwamba hutoka mkononi mwa Mungu.


Siku ya kufanikiwa ufurahi, Na siku ya mabaya ufikiri. Mungu ameifanya hiyo moja kwenda sambamba na hiyo ya pili, ili mwanadamu asipate kulijua neno lolote litakalofuata baada yake.


Mara malaika wa Bwana akampiga, kwa sababu hakumpa Mungu utukufu; akaliwa na wadudu, akatokwa na roho.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo