Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Mhubiri 3:20 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

20 Wote huendea mahali pamoja; wote hutoka katika mavumbi; na hata mavumbini hurudi tena.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

20 Wote hufa na kwenda mahali pamoja. Wote wametoka mavumbini; na wote watarudi mavumbini,

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

20 Wote hufa na kwenda mahali pamoja. Wote wametoka mavumbini; na wote watarudi mavumbini,

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

20 Wote hufa na kwenda mahali pamoja. Wote wametoka mavumbini; na wote watarudi mavumbini,

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

20 Wote huenda mahali panapofanana; wote hutoka mavumbini, mavumbini wote hurudi.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

20 Wote huenda mahali panapofanana; wote hutoka mavumbini, mavumbini wote hurudi.

Tazama sura Nakili




Mhubiri 3:20
20 Marejeleo ya Msalaba  

Ishmaeli aliishi miaka mia moja na thelathini na saba. Akakata roho, akafa, akakusanyika kwa watu wake.


Abrahamu akafariki, naye akafa katika uzee mwema, mzee sana, ameshiba siku, akakusanyika kwa watu wake.


kwa jasho la uso wako utakula chakula, hata utakapoirudia ardhi, ambayo katika hiyo ulitwaliwa; kwa maana u mavumbi wewe, nawe mavumbini utarudi.


Lakini mwanadamu hufa, hufariki dunia; Naam, mwanadamu hukata roho, naye yupo wapi?


Mtu akifa, je! Atakuwa hai tena? Mimi ningengoja siku zote za huduma yangu, Hadi kufunguliwa kwangu kunifikie.


Nikitazamia kuzimu kuwa nyumba yangu; Nikitandika malazi yangu gizani;


Je! Mtu katika kuanguka kwake hanyoshi mkono? Na kulilia msaada katika msiba wake?


Wenye mwili wote wangeangamia pamoja, Nao wanadamu watarejea tena kuwa mavumbi.


Kama vile wingu likomavyo na kutoweka, Ndivyo alivyo huyo ashukaye kuzimuni, hatazuka tena kabisa.


Kwa maana Yeye anatujua umbo letu, Na kukumbuka ya kuwa sisi tu mavumbi.


Wewe wauficha uso wako, Wao wanafadhaika; Waiondoa pumzi yao, wanakufa, Na kuyarudia mavumbi yao,


Kama kondoo wamewekwa kwenda kuzimu, Na kifo kitakuwa mchungaji wao; Watu wanyofu watawamiliki asubuhi; Miili yao itaoza, kao lao ni kuzimu.


Nayo mavumbi kuirudia nchi kama yalivyokuwa, Nayo roho kumrudia Mungu aliyeitoa.


Ni nani ajuaye kama roho ya binadamu huenda juu, na kama roho ya mnyama huenda chini?


naam, ajapoishi miaka elfu mara mbili, asijiburudishe kwa mema; je! Wote hawaendi mahali pamoja?


Heri kuiendea nyumba ya matanga, Kuliko kuiendea nyumba ya karamu. Kwa maana huo ndio mwisho wa wanadamu wote, naye aliye hai atautia moyoni mwake.


Lolote mkono wako utakalolipata kulifanya, ulifanye kwa nguvu zako; kwa kuwa hakuna kazi, wala shauri, wala maarifa, wala hekima, huko kuzimu uendako wewe.


Tena, wengi wa hao wanaolala katika mavumbi ya nchi wataamka, wengine wapate uzima wa milele, wengine aibu na kudharauliwa milele.


Na ukiisha kuiona, wewe nawe utakusanyika pamoja na baba zako, kama Haruni ndugu yako alivyokusanyika;


Tufuate:

Matangazo


Matangazo