Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Mhubiri 10:12 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

12 Maneno ya kinywa chake mwenye hekima yana neema; Bali midomo ya mpumbavu itammeza nafsi yake.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

12 Maneno ya mwenye hekima humnufaisha asemaye; lakini midomo ya mpumbavu humwangamiza.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

12 Maneno ya mwenye hekima humnufaisha asemaye; lakini midomo ya mpumbavu humwangamiza.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

12 Maneno ya mwenye hekima humnufaisha asemaye; lakini midomo ya mpumbavu humwangamiza.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

12 Maneno yanayotoka kinywani mwa mtu mwenye hekima yana neema, bali mpumbavu huangamizwa na midomo yake mwenyewe.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

12 Maneno yatokayo kinywani mwa mtu mwenye hekima yana neema, bali mpumbavu huangamizwa na midomo yake mwenyewe.

Tazama sura Nakili




Mhubiri 10:12
36 Marejeleo ya Msalaba  

Daudi akamwambia, Damu yako na iwe juu ya kichwa chako mwenyewe; maana umejishuhudia nafsi yako ukisema, Nimemwua masihi wa BWANA.


Lakini ningewatia nguvu kwa kinywa changu, Na maliwazo ya midomo yangu yangewatuliza.


Nao wainuapo vichwa watu wanaonizunguka, Madhara ya midomo yao yawafunike.


Kinywa chake mwenye haki hunena hekima, Na ulimi wake husema hukumu.


Kwa ajili ya ulimi wao wataangamizwa; Wote wawaonao watatetemeka kwa hofu. Wote wawaonao watatikisa kichwa.


Akonyezaye kwa jicho huleta masikitiko; Bali mpumbavu mwenye maneno mengi ataanguka.


Aliye na akili moyoni mwake atapokea agizo; Bali mpumbavu mwenye maneno mengi ataanguka.


Kuna anenaye bila kufikiri, kama kuchoma kwa upanga; Bali ulimi wa mwenye haki ni afya.


Ulimi wa mwenye hekima hutamka maarifa vizuri; Bali vinywa vya wapumbavu humwaga upumbavu.


Mtu hulifurahia jibu la kinywa chake; Na neno linenwalo wakati wa kufaa ni jema kama nini!


Shahidi wa uongo hakosi ataadhibiwa; Wala asemaye uongo hataokoka.


Apendaye usafi wa moyo, na neema ya midomo; Mfalme atakuwa rafiki yake.


Kama mwiba uingiao katika mkono wa mlevi; Kadhalika mithali katika kinywa cha mpumbavu.


Hufumbua kinywa chake kwa hekima, Na sheria ya wema iko katika ulimi wake.


Maneno yao wenye hekima huwa mfano wa michokoo; na kama misumari iliyogongomewa sana; ndivyo yalivyo maneno yao walio wakuu wa makusanyiko, ambayo yatoka kwa mchungaji mmoja.


Mpumbavu huikunja mikono yake, Naye hula chakula chake mwenyewe;


Usiseme maneno ya ujinga kwa kinywa chako, wala moyo wako usiwe na haraka kunena mbele za Mungu; kwa maana, Mungu yuko mbinguni, na wewe upo chini, Kwa hiyo maneno yako na yawe machache.


Usikiache kinywa chako kuukosesha mwili wako; wala usiseme mbele ya huyo malaika ya kwamba hukukusudia; kwa nini Mungu akasirishwe na maneno yako, na kuiharibu kazi ya mikono yako?


Maneno ya wenye hekima yanenwayo taratibu husikiwa, Zaidi ya mlio wake atawalaye katikati ya wapumbavu.


Mtu mwema katika akiba njema hutoa mema; na mtu mbaya katika akiba mbaya hutoa mabaya.


Akamwambia, Nitakuhukumu kwa kinywa chako, mtumwa mwovu wewe. Ulinijua kuwa ni mtu mgumu, nichukuaye nisichoweka, na kuvuna nisichopanda;


Wakamshuhudia wote, wakiyastaajabia maneno ya neema yaliyotoka kinywani mwake, wakasema, Huyu siye mwana wa Yusufu?


Neno lolote lililo ovu lisitoke vinywani mwenu, bali lililo jema la kumfaa mwenye kuhitaji, ili liwape neema wanaosikia.


Maneno yenu yawe na neema siku zote, yakikolezwa chumvi, ili mpate kujua jinsi iwapasavyo kumjibu kila mtu.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo