Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Methali 31:17 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

17 Hujifunga nguvu viunoni kama mshipi; Hutia mikono yake nguvu.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

17 Huwa tayari kufanya kazi kwa nguvu na kuiimarisha mikono yake.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

17 Huwa tayari kufanya kazi kwa nguvu na kuiimarisha mikono yake.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

17 Huwa tayari kufanya kazi kwa nguvu na kuiimarisha mikono yake.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

17 Hufanya kazi zake kwa nguvu, mikono yake ina nguvu kwa ajili ya kazi zake.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

17 Hufanya kazi zake kwa nguvu, mikono yake ina nguvu kwa ajili ya kazi zake.

Tazama sura Nakili




Methali 31:17
12 Marejeleo ya Msalaba  

Lakini upinde wake ukakaa imara, Mikono yake ikapata nguvu, Kwa mikono ya Mwenye Enzi wa Yakobo; Kwa jina la mchungaji, yeye mwamba wa Israeli,


Mkono wa BWANA ulikuwa juu ya Eliya; akajikaza viuno, akapiga mbio akatangulia Ahabu mpaka kuiingia Yezreeli.


Ndipo Elisha akamwambia Gehazi, Jikaze viuno, ukachukue fimbo yangu mkononi mwako, ukaende zako; ukikutana na mtu, usimsalimu; na mtu akikusalimu, usimjibu; ukaweke fimbo yangu juu ya uso wa mtoto.


Basi jifunge viuno kama mwanamume, Maana nitakuuliza neno, nawe niambie.


Huangalia shamba, akalinunua; Kwa mapato ya mikono yake hupanda mizabibu.


Huona kama bidhaa yake ina faida; Taa yake haizimiki usiku.


Mfua chuma hufanza shoka, hufanya kazi kwa makaa, huitengeneza sanamu kwa nyundo, huifanyiza kwa nguvu za mkono wake; naam, huona njaa, nguvu zake zikampungukia; asipokunywa maji huzimia.


Ingawa nimewafundisha na kuwatia nguvu mikono yao, hata hivyo hukusudia udhalimu juu yangu.


Viuno vyenu na viwe vimefungwa, na taa zenu ziwe zinawaka;


Hatimaye, mzidi kuwa hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu zake.


Basi simameni, mkiwa mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani,


Kwa hiyo iweni tayari, na makini; mkiitumainia kwa utimilifu ile neema mtakayoletewa katika ufunuo wake Yesu Kristo.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo