Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Methali 27:8 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

8 Kama ndege aendaye huku na huko mbali na kitundu chake; Ndivyo alivyo mtu aendaye huku na huko mbali na mahali pake.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

8 Mtu aliyepotea mbali na kwake, ni kama ndege aliyepotea mbali na kiota chake.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

8 Mtu aliyepotea mbali na kwake, ni kama ndege aliyepotea mbali na kiota chake.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

8 Mtu aliyepotea mbali na kwake, ni kama ndege aliyepotea mbali na kiota chake.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

8 Kama ndege atangatangavyo mbali na kiota chake, ndivyo alivyo mtu atangatangaye mbali na nyumbani mwake.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

8 Kama ndege atangatangavyo mbali na kiota chake, ndivyo alivyo mtu atangatangaye mbali na nyumbani mwake.

Tazama sura Nakili




Methali 27:8
17 Marejeleo ya Msalaba  

Abrahamu akaamka asubuhi na mapema akatwaa mkate na kiriba cha maji, akampa Hajiri akamtwika begani pake, na kijana, akamruhusu; naye akatoka, akapotea katika jangwa la Beer-sheba.


Kaini akatoka mbele za uso wa BWANA, akakaa katika nchi ya Nodi, Mashariki mwa Edeni.


Farao akamwambia, Umekosa nini kwangu, hata, tazama, unatafuta kuirudia nchi yako? Akajibu, Hakuna, lakini unipe ruhusa tu.


Akafika kunako pango, akalala ndani yake. Na tazama, neno la BWANA likamjia, naye akamwambia, Unafanya nini hapa, Eliya?


Mtu aikosaye njia ya busara Atakaa katika mkutano wao waliokufa.


Kama shomoro katika kutangatanga kwake, Na kama mbayuwayu katika kuruka kwake; Kadhalika laana isiyo na sababu haimpati mtu.


Nafsi iliyoshiba hukinai sega la asali; Bali nafsi yenye njaa huona kila kitu kichungu kuwa kitamu.


Na binti za Moabu watakuwa kama ndege warukao huku na huko, kama kiota cha ndege waliotiwa hofu, kwenye vivuko vya Arnoni.


Lakini Yona akaondoka akimbilie Tarshishi, apate kujiepusha na uso wa BWANA; akateremka hadi Yafa, akaona merikebu inayokwenda Tarshishi; basi, akalipa nauli, akapanda merikebuni, aende pamoja nao Tarshishi, ajiepushe na uso wa BWANA.


Kila mtu na akae katika hali ile ile ambayo alikuwa nayo alipoitwa.


ni mawimbi ya bahari yasiyozuilika, yakitoa aibu yao wenyewe kama povu; ni nyota zipoteazo, ambao weusi wa giza ndio akiba yao waliowekewa milele.


Kisha nabii Gadi akamwambia Daudi, Usikae hapa ngomeni; ondoka, ukaende mpaka nchi ya Yuda. Ndipo Daudi akaondoka, akaenda zake, akakaa katika msitu wa Herethi.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo