Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Methali 25:21 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

21 Adui yako akiwa ana njaa, mpe chakula; Tena akiwa ana kiu, mpe maji ya kunywa;

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

21 Adui yako akiwa na njaa, mpe chakula; akiwa na kiu, mpe maji ya kunywa.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

21 Adui yako akiwa na njaa, mpe chakula; akiwa na kiu, mpe maji ya kunywa.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

21 Adui yako akiwa na njaa, mpe chakula; akiwa na kiu, mpe maji ya kunywa.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

21 Kama adui yako ana njaa, mpe chakula ale; kama ana kiu, mpe maji anywe.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

21 Kama adui yako ana njaa, mpe chakula ale; kama ana kiu, mpe maji anywe.

Tazama sura Nakili




Methali 25:21
11 Marejeleo ya Msalaba  

Akamjibu, Usiwapige; je! Ungetaka kuwapiga watu ambao umewatwaa mateka kwa upanga wako na uta wako? Weka chakula na maji mbele yao, wapate kula na kunywa, na kwenda kwa bwana wao.


Wakaondoka wale watu waliotajwa majina yao, wakawatwaa wafungwa, wakawavika kwa zile nyara wale wote waliokuwa uchi, wakawapa mavazi na viatu, wakawalisha, wakawanywesha, wakawatia mafuta, wakawapandisha waliokuwa dhaifu miongoni mwao juu ya punda wakawaleta Yeriko, mji wa mitende, kwa ndugu zao; kisha wakarudi Samaria.


Huwapa usalama, nao wapumzika kwao; Na macho yake yako juu ya njia zao.


Usifurahi, adui yako aangukapo; Wala moyo wako usishangilie ajikwaapo;


Usiseme, Nitamtenda kama alivyonitenda mimi; Nitamlipa mtu huyo sawasawa na tendo lake.


Amwimbiaye nyimbo mtu mwenye moyo mzito, Ni kama yeye avuaye nguo wakati wa baridi; Ni kama siki juu ya magadi.


lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi,


Na sasa, angalia, ninajua ya kuwa hakika utakuwa mfalme, na ufalme wa Israeli utafanyika imara mkononi mwako.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo