Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Mathayo 10:7 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

7 Na katika kuenda kwenu, hubirini, mkisema, Ufalme wa mbinguni umekaribia.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

7 Mnapokwenda hubirini hivi: ‘Ufalme wa mbinguni umekaribia.’

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

7 Mnapokwenda hubirini hivi: ‘Ufalme wa mbinguni umekaribia.’

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

7 Mnapokwenda hubirini hivi: ‘Ufalme wa mbinguni umekaribia.’

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

7 Mnapoenda, hubirini ujumbe huu, ‘Ufalme wa mbinguni umekaribia.’

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

7 Wakati mnapokwenda, hubirini mkisema, ‘Ufalme wa Mbinguni umekaribia.’

Tazama sura Nakili




Mathayo 10:7
19 Marejeleo ya Msalaba  

Roho ya Bwana MUNGU i juu yangu; kwa sababu BWANA amenitia mafuta niwahubirie wanyenyekevu habari njema; amenituma ili kuwatibu waliovunjika moyo, kuwatangazia mateka uhuru wao, na hao waliofungwa habari za kufunguliwa kwao.


Ponyeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo; mmepata bure, toeni bure.


Ikawa Yesu alipokwisha kuwaagiza wanafunzi wake kumi na wawili, alitoka huko kwenda kufundisha na kuhubiri katika miji yao.


Je! Katika hao wawili ni yupi aliyefanya mapenzi ya babaye? Wakamwambia, Ni yule wa kwanza. Basi Yesu akawaambia, Amin nawaambia, watoza ushuru na makahaba wanatangulia mbele yenu kuingia katika ufalme wa Mungu.


Kwa sababu hiyo nawaambia, Ufalme wa Mungu utaondolewa kwenu, nao watapewa taifa lingine lenye kuzaa matunda yake.


Ole wenu Waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnawafungia watu ufalme wa mbinguni; ninyi wenyewe hamwingii, wala wanaoingia hamwaachi waingie.


Tubuni; kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia.


Tokea wakati huo Yesu alianza kuhubiri, na kusema, Tubuni; kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia.


Wakatoka, wakahubiri kwamba watu watubu.


Torati na Manabii vilikuwapo mpaka Yohana; tangu wakati huo Habari Njema ya ufalme wa Mungu hutangazwa, na kila mtu hujiingiza kwa nguvu.


Akawatuma wautangaze ufalme wa Mungu, na kuponya wagonjwa.


Wakaenda, wakazunguka katika vijiji, wakihubiri Injili, na kuponya watu magonjwa kila mahali.


Akamwambia Waache wafu wawazike wafu wao; bali wewe nenda ukautangaze ufalme wa Mungu.


Huyo alimjia usiku, akamwambia, Rabi, tunajua ya kuwa u mwalimu, umetoka kwa Mungu; kwa maana hakuna mtu awezaye kuzifanya ishara hizi uzifanyazo wewe, isipokuwa Mungu yu pamoja naye.


Petro alipokuwa akiingia Kornelio akatoka amlaki akamwangukia miguuni mwake, akamsujudia.


akihubiri habari za ufalme wa Mungu, na kuyafundisha mambo ya Bwana Yesu Kristo, kwa ujasiri mwingi, asikatazwe na mtu.


wakifadhaika sana kwa sababu wanawafundisha watu na kuhubiri kuwa katika Yesu kuna ufufuo wa wafu.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo