Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Matendo 9:35 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

35 Na watu wote waliokaa Lida na Sharoni wakamwona, wakamgeukia Bwana.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

35 Wakazi wote wa Luda na Saroni walimwona Ainea, na wote wakamgeukia Bwana.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

35 Wakazi wote wa Luda na Saroni walimwona Ainea, na wote wakamgeukia Bwana.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

35 Wakazi wote wa Luda na Saroni walimwona Ainea, na wote wakamgeukia Bwana.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

35 Watu wote wa Lida na Sharoni walipomwona Ainea akitembea wakamgeukia Bwana Isa.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

35 Watu wote wa Lida na Sharoni walipomwona Ainea akitembea wakamgeukia Bwana Isa.

Tazama sura Nakili




Matendo 9:35
32 Marejeleo ya Msalaba  

na juu ya mifugo iliyolishwa katika Sharoni alikuwa Shitrai, Msharoni; na juu ya mifugo iliyokuwamo mabondeni alikuwa Shafati mwana wa Adlai;


Nao wakakaa huko Gileadi, katika Bashani, na katika miji yake, na katika viunga vyote vya Sharoni, hadi mipakani mwake.


Na wana wa Elpaali; Eberi, na Mishamu, na Shemedi, ambaye ndiye aliyejenga Ono na Lodi, pamoja na vijiji vyake;


Watu wa Lodi, na Hadidi, na Ono, mia saba ishirini na watano.


Lodi, na Ono, lililokuwa bonde la mafundi.


Wana wa Lodi, na Hadidi, na Ono, mia saba ishirini na mmoja.


Watu wako watajitoa kwa hiari, Siku ya uwezo wako; Kwa uzuri wa utakatifu, Tokea tumbo la asubuhi, Unao umande wa ujana wako.


Miisho yote ya dunia itakumbuka, Na watu watamrejea BWANA; Jamaa zote za mataifa watamsujudia.


Mwelekeeni yeye mliyemwasi sana, enyi wana wa Israeli.


Nchi inaomboleza, na kulegea; Lebanoni imetahayarika na kunyauka; Sharoni imekuwa kama jangwa; Bashani na Karmeli zimepukutika majani.


Litachanua maua mengi, na kufurahi, naam, kwa shangwe na kuimba; litapewa uzuri wa Lebanoni, utukufu wa Karmeli na Sharoni; watauona utukufu wa BWANA, ukuu wa Mungu wetu.


Na Sharoni itakuwa zizi la makundi ya kondoo, na bonde la Akori mahali pa kulala makundi ya ng'ombe, kwa ajili ya watu wangu walionitafuta.


Ni nani aliyesikia neno kama hili? Ni nani aliyeona mambo kama haya? Je! Nchi yaweza kuzaliwa kwa siku moja? Taifa laweza kuzaliwa mara? Maana Sayuni, mara alipopata uchungu, Alizaa watoto wake.


Na tuchunguze njia zetu na kuzijaribu, Na kumrudia BWANA tena.


Basi, mrudie Mungu wako; shika fadhili na hukumu; ukamngojee Mungu wako daima.


Chukueni maneno pamoja nanyi, mkamrudie BWANA; mkamwambie, Ondoa maovu yote, uyatakabali yaliyo mema; na hivyo ndivyo mtakavyotoa sadaka za midomo yetu kana kwamba ni ng'ombe.


rarueni mioyo yenu, wala si mavazi yenu, mkamrudie BWANA, Mungu wenu; kwa maana yeye ndiye mwenye neema, amejaa huruma; si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa rehema, naye hughairi kuadhibu.


Mkono wa Bwana ukawa pamoja nao, watu wengi wakaamini, wakamwelekea Bwana.


Kwa sababu hiyo mimi naamua hivi; Tusiwataabishe wale waliomgeukia Mungu katika Mataifa;


Mambo haya yakaendelea kwa muda wa miaka miwili, hata wote waliokaa Asia wakalisikia neno la Bwana, Wayahudi kwa Wagiriki.


Hivyo ndivyo neno la Bwana lilivyozidi na kushinda kwa nguvu.


wakimsifu Mungu, na kuwapendeza watu wote. Bwana akalizidisha kanisa kila siku kwa wale waliokuwa wakiokolewa.


Lakini wengi katika hao waliosikia lile neno waliamini; na hesabu ya wanaume ikawa kama elfu tano.


Neno la Mungu likaenea; na hesabu ya wanafunzi ikazidi sana katika Yerusalemu; jamii kubwa ya makuhani wakaitii ile Imani.


Petro akamwambia, Ainea, Yesu Kristo akuponya; inuka, ujitandikie. Mara akainuka.


Ikajulikana katika mji mzima wa Yafa; watu wengi wakamwamini Bwana.


Lakini wakati wowote watakapomgeukia Bwana, ule utaji huondolewa.


Na wakati uwapo katika mashaka, ukiisha kupatwa na mambo haya yote, siku za mwisho, utamrudia BWANA, Mungu wako, na kuisikiza sauti yake;


Tufuate:

Matangazo


Matangazo