Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Matendo 20:36 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

36 Alipokwisha kunena haya akapiga magoti, akaomba pamoja nao wote.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

36 Baada ya kusema hayo, Paulo alipiga magoti pamoja nao wote, akasali.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

36 Baada ya kusema hayo, Paulo alipiga magoti pamoja nao wote, akasali.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

36 Baada ya kusema hayo, Paulo alipiga magoti pamoja nao wote, akasali.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

36 Paulo alipomaliza kusema haya akapiga magoti pamoja nao wote akaomba.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

36 Paulo alipomaliza kusema haya akapiga magoti pamoja nao wote akaomba.

Tazama sura Nakili




Matendo 20:36
9 Marejeleo ya Msalaba  

(maana Sulemani alikuwa amefanya mimbari ya shaba, urefu wake dhiraa tano, na upana wake dhiraa tano, na kwenda juu kwake dhiraa tatu, na kuisimamisha katikati ya ua; akasimama juu yake, akapiga magoti mbele ya mkutano wote wa Israeli, akaikunjua mikono yake kuelekea mbinguni);


Hata Danieli, alipojua ya kuwa yale maandiko yamekwisha kutiwa sahihi, akaingia nyumbani mwake, (na madirisha katika chumba chake yalikuwa yamefunguliwa kuelekea Yerusalemu;) akapiga magoti mara tatu kila siku, akasali, akashukuru mbele za Mungu wake, kama alivyokuwa akifanya tokea hapo.


Mwenyewe akajitenga nao kama kiasi cha kutupa jiwe, akapiga magoti akaomba,


Katika mambo yote nimewaonesha ya kuwa kwa kushika kazi hivi imewapasa kuwasaidia wanyonge, na kuyakumbuka maneno ya Bwana Yesu, jinsi alivyosema mwenyewe, Ni heri kutoa kuliko kupokea.


Hata tulipotimiza siku zile tukaondoka tukaenda zetu, na watu wote, pamoja na wake zao na watoto wao, wakatusindikiza mpake nje ya mji, tukapiga magoti pwani tukaomba;


Akapiga magoti, akalia kwa sauti kuu, Bwana, usiwahesabie dhambi hii. Akiisha kusema haya akalala. Na Sauli alikuwa akiona kitendo cha kuuawa kwake kuwa sawa.


Petro akawatoa nje wote, akapiga magoti, akaomba, kisha akaelekea yule maiti, akanena, Tabitha, inuka. Naye akafumbua macho yake, na alipomwona Petro akajiinua, akaketi.


Kwa hiyo nampigia Baba magoti,


Msijisumbue kwa neno lolote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo