Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Marko 8:2 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

2 Nawahurumia mkutano kwa sababu yapata siku tatu wamekaa nami, wala hawana kitu cha kula;

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

2 “Nawaonea huruma watu hawa kwa sababu wamekuwa nami kwa siku tatu, wala hawana chakula.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

2 “Nawaonea huruma watu hawa kwa sababu wamekuwa nami kwa siku tatu, wala hawana chakula.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

2 “Nawaonea huruma watu hawa kwa sababu wamekuwa nami kwa siku tatu, wala hawana chakula.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

2 “Ninahurumia umati huu wa watu, kwa sababu sasa wamekuwa nami kwa muda wa siku tatu na hawana chakula.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

2 “Ninauhurumia huu umati wa watu, kwa sababu sasa wamekuwa nami kwa muda wa siku tatu na hawana chakula.

Tazama sura Nakili




Marko 8:2
23 Marejeleo ya Msalaba  

Akatazama, kumbe! Pana mkate umeokwa juu ya makaa, na gudulia la maji, kichwani pake. Akala, akanywa, akajinyosha tena.


Kama vile baba awahurumiavyo watoto wake, Ndivyo BWANA anavyowahurumia wamchao.


Macho ya watu wote yakuelekea Wewe, Nawe huwapa chakula chao wakati wake.


BWANA ni mwenye fadhili na huruma, Si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa rehema,


Atarejea na kutuhurumia; atayakanyaga maovu yetu; nawe utazitupa dhambi zao zote katika vilindi vya bahari.


Yesu akatoka, akaona mkutano mkuu, akawahurumia, akawaponya wagonjwa wao.


Yesu akawahurumia, akawagusa macho yao; mara wakapata kuona, wakamfuata.


Na alipowaona makutano, aliwahurumia, kwa sababu walikuwa wamechoka na kutawanyika kama kondoo wasio na mchungaji.


Naye akamhurumia, akanyosha mkono wake, akamgusa, akamwambia, Nataka, takasika.


lakini hakumruhusu, bali alimwambia, Nenda zako nyumbani kwako, kwa watu wa kwenu, kawahubirie ni mambo gani makuu aliyokutendea Bwana, na jinsi alivyokurehemu.


Wakaenda zao faragha mashuani, mahali pasipokuwa na watu.


Naye aliposhuka mashuani, akaona mkutano mkuu, akawahurumia; kwa sababu walikuwa kama kondoo wasio na mchungaji; akaanza kuwafundisha mambo mengi.


nami nikiwaaga waende zao nyumbani kwao wakiwa na njaa, watazimia njiani; na baadhi yao wametoka mbali.


Na mara nyingi amemtupa katika moto, na katika maji, amwangamize; lakini ukiweza neno lolote, utuhurumie, na kutusaidia.


Akaondoka, akaenda kwa babaye. Alipokuwa bado mbali, baba yake alimwona, akamwonea huruma, akaenda mbio akamwangukia shingoni, akambusu.


Bwana alipomwona alimwonea huruma, akamwambia, Usilie.


Hivyo ilimpasa kufananishwa na ndugu zake katika mambo yote, apate kuwa kuhani mkuu mwenye rehema, mwaminifu katika mambo ya Mungu, ili afanye kafara ya suluhu kwa dhambi za watu wake.


Kwa kuwa hamna kuhani mkuu asiyeweza kuchukuana nasi katika mambo yetu ya udhaifu; bali yeye alijaribiwa kama sisi katika mambo yote, bila kufanya dhambi.


awezaye kuwachukulia kwa upole wao wasiojua na wenye kupotea, kwa kuwa yeye mwenyewe ana udhaifu;


Tufuate:

Matangazo


Matangazo