Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Kutoka 7:23 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

23 Farao akazunguka na kuingia nyumbani mwake, wala hata hilo hakuliweka moyoni.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

23 Basi, Farao akarudi nyumbani kwake, na hata haya yaliyotokea hakuyajali.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

23 Basi, Farao akarudi nyumbani kwake, na hata haya yaliyotokea hakuyajali.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

23 Basi, Farao akarudi nyumbani kwake, na hata haya yaliyotokea hakuyajali.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

23 Badala yake, Farao akageuka, akaenda kwenye jumba lake la kifalme, wala hakulitia hili moyoni.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

23 Badala yake, Farao akageuka, akaenda kwenye jumba lake la kifalme, wala hakulitia hili moyoni.

Tazama sura Nakili




Kutoka 7:23
20 Marejeleo ya Msalaba  

Je! Mtu ni kitu gani, hata ukamtukuza, Na kumtia moyoni mwako,


Msiitumainie dhuluma, Wala msijivune kwa unyang'anyi; Mali izidipo msiiangalie sana moyoni.


Lakini waganga wa Misri wakafanya mfano wa hayo kwa uganga wao; na moyo wake Farao ukawa mgumu, wala hakuwasikiza, kama BWANA alivyonena.


Wamisri wote wakachimbachimba kando ya mto ili wapate maji ya kunywa; maana, hawakuweza kuyanywa yale maji ya mtoni.


Yeye aliyelicha neno la BWANA miongoni mwa watumishi wa Farao aliwakimbiza watumishi wake na wanyama wake waingie nyumbani;


na yeye asiyelitia moyoni neno la BWANA akawaacha watumishi wake na wanyama wake mashambani.


Tega sikio lako uyasikie maneno ya wenye hekima, na kuuelekeza moyo wako kwa maarifa yangu;


Ndipo nilipoangalia na kufikiri sana; Niliona, nikapata mafundisho.


Mwanadamu mwenye kicho yu heri sikuzote; Bali mshupavu wa moyo ataangukia madhara.


Aonywaye mara nyingi akishupaza shingo, Atavunjika ghafla, wala hapati dawa.


BWANA, mkono wako umeinuliwa, lakini hawaoni; lakini watauona wivu wako kwa ajili ya watu wako, nao watatahayari; naam, moto utawala adui zako.


Ukasema, Mimi nitakuwa malkia milele; hata hukuyatia hayo moyoni mwako, wala hukukumbuka mwisho wa mambo hayo.


Lakini hawakuogopa, wala hawakurarua mavazi yao, wala mfalme, wala watumishi wake hata mmoja waliosikia maneno hayo yote.


Ee BWANA, macho yako je! Hayaangalii uaminifu? Umewapiga, lakini hawakuhuzunika; umewakomesha, lakini wamekataa kurudiwa wamefanya nyuso zao kuwa ngumu kuliko mwamba wamekataa kurudi.


Mtu yule akaniambia, Mwanadamu, tazama kwa macho yako, sikia kwa masikio yako, ukaweke moyoni mwako, yote nitakayokuonesha; maana umeletwa hapa kusudi nikuoneshe haya; tangaza habari ya yote utakayoyaona kwa nyumba ya Israeli.


Angalieni, enyi mlio kati ya mataifa, katazameni, kastaajabuni sana; kwa maana mimi natenda tendo siku zenu, ambalo hamtaliamini hata mkiambiwa.


Kama hamtaki kusikia, na kama hamtaki kuitia moyoni, ili kulitukuza jina langu, asema BWANA wa majeshi, basi nitawaleteeni laana, nami nitazilaani baraka zenu; naam, nimekwisha kuzilaani, kwa sababu hamyatii haya moyoni.


akawaambia, Yawekeni mioyoni mwenu maneno yote ambayo nashuhudia kwenu hivi leo; nayo waamuruni watoto wenu, wayatunze na kuyafanya maneno yote ya torati hii.


Na alipokuwa karibu kufa, wale wanawake waliokuwa wakimuhudumia wakamwambia, Usiogope; kwa maana umezaa mtoto wa kiume. Lakini hakujibu, wala hakumtazama.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo