Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Kutoka 23:8 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

8 Nawe usipokee rushwa; kwani hiyo rushwa huwapofusha macho hao waonao, na kuyapotoa maneno ya wenye haki.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

8 Usipokee rushwa, maana rushwa huwapofusha wakuu na kupotosha mambo ya wenye haki.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

8 Usipokee rushwa, maana rushwa huwapofusha wakuu na kupotosha mambo ya wenye haki.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

8 Usipokee rushwa, maana rushwa huwapofusha wakuu na kupotosha mambo ya wenye haki.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

8 “Usipokee rushwa, kwa kuwa rushwa hupofusha wale waonao, na kupinda maneno ya wenye haki.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

8 “Usipokee rushwa, kwa kuwa rushwa hupofusha wale waonao, na kupinda maneno ya wenye haki.

Tazama sura Nakili




Kutoka 23:8
20 Marejeleo ya Msalaba  

Asiyetoa fedha yake apate kula riba, Asiyepokea rushwa amwangamize asiye na hatia. Mtu atendaye mambo hayo Hataondoshwa milele.


Mikononi mwao mna madhara, Na mkono wao wa kulia umejaa rushwa.


Atamaniye faida huifadhaisha nyumba yake mwenyewe; Bali achukiaye zawadi ataishi.


Asiye haki hutoa rushwa kifuani, Ili kuzipotosha njia za hukumu.


Kipawa ni kama kito cha thamani machoni pake yeye aliye nacho; Kila kigeukapo hufanikiwa.


Utajiri huongeza marafiki wengi; Bali maskini hutengwa na rafiki yake.


Kweli jeuri humpumbaza mwenye hekima, Na rushwa huuharibu ufahamu.


Msilete tena matoleo ya ubatili; uvumba ni chukizo kwangu; mwezi mwandamo na sabato, kuita makutano; siyawezi maovu hayo na makutano ya ibada.


Wakuu wako ni waasi, na rafiki za wezi; kila mtu hupenda rushwa, hufuata malipo; hawampatii yatima haki yake, wala maneno ya mjane hayawafikii.


Ni yeye aendaye kwa haki, anenaye maneno ya adili; ni yeye anayedharau faida ipatikanayo kwa dhuluma; akung'utaye mikono yake asipokee rushwa; azibaye masikio yake asisikie habari za umwagaji wa damu; afumbaye macho yake asitazame uovu.


Ole wao walio hodari kunywa kileo chenye nguvu, na walio hodari wa kuchanganya vileo;


wampao haki mwenye uovu, ili wapewe ijara, na kumwondolea mwenye haki haki yake!


Ndani yako wamepokea rushwa ili kumwaga damu; umepokea riba na faida; nawe kwa choyo umepata mapato kwa kuwadhulumu jirani zako, nawe umenisahau mimi, asema Bwana MUNGU.


Kileo chao kimegeuka kuwa uchungu; huzini daima; wakuu wake hupenda aibu.


Maana mimi najua jinsi maasi yenu yalivyo mengi, na jinsi dhambi zenu zilivyo kubwa; ninyi mnaowaonea wenye haki, mnaopokea rushwa, na kuwageuza wahitaji langoni wasipate haki yao.


Mikono yao ni hodari kwa kutenda maovu; afisa na hakimu wanataka rushwa, mtu mkubwa hunena madhara yaliyomo rohoni mwake; hivyo ndivyo wayafumavyo hayo pamoja.


Kwa maana BWANA, Mungu wenu, yeye ndiye Mungu wa miungu, na Bwana wa mabwana, Mungu mkuu, mwenye kuogofya, asiyependelea watu, wala kukubali rushwa.


Usipotoe maamuzi; wala usipendelee uso wa mtu; wala usitwae rushwa; kwa kuwa rushwa hupofusha macho ya wenye akili, na kugeuza kesi wa wenye haki.


Nami nipo hapa; basi, mnishuhudie mbele za BWANA, na mbele ya masihi wake, nilitwaa ng'ombe wa nani? Au nilitwaa punda wa nani? Au ni nani niliyemdhulumu? Ni nani niliyemwonea? Au kwa mkono wa nani nimepokea rushwa inipofushe macho? Nami nitawarudishia ninyi.


Ila wanawe hawakuenda katika njia zake, bali waliziacha, ili wapate faida; wakapokea rushwa, na kupotosha hukumu.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo