Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Kutoka 21:14 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

14 Lakini, mtu akimwendea mwenziwe kwa kujikinai, kusudi apate kumwua kwa hila; huyo utamwondoa hata madhabahuni pangu, auawe.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

14 Lakini mtu akimshambulia mwenzake makusudi na kumwua kwa ujeuri, hata kama atakimbilia kwenye madhabahu, mtamtoa huko madhabahuni pangu na kumwua.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

14 Lakini mtu akimshambulia mwenzake makusudi na kumwua kwa ujeuri, hata kama atakimbilia kwenye madhabahu, mtamtoa huko madhabahuni pangu na kumwua.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

14 Lakini mtu akimshambulia mwenzake makusudi na kumwua kwa ujeuri, hata kama atakimbilia kwenye madhabahu, mtamtoa huko madhabahuni pangu na kumwua.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

14 Lakini kama mtu akipanga na kumuua mwingine kwa makusudi, mwondoe katika madhabahu yangu na kumuua.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

14 Lakini kama mtu akipanga na kumuua mwingine kwa makusudi, mwondoe katika madhabahu yangu na kumuua.

Tazama sura Nakili




Kutoka 21:14
18 Marejeleo ya Msalaba  

Basi Abneri alipokuwa amerudi Hebroni, Yoabu akamchukua kando hadi katikati ya lango, ili aseme naye kwa faragha; akampiga mkuki wa tumbo huko, hadi akafa; kwa ajili ya damu ya Asaheli, ndugu yake.


Naye Yehoyada kuhani akawaamuru wakuu wa mamia, majemadari wa jeshi, akawaambia, Mtoeni kati ya safu; naye yeyote amfuataye mwueni kwa upanga. Kwani kuhani akasema, Asiuawe nyumbani mwa BWANA.


Umzuie mtumishi wako asitende mambo ya kiburi, Yasinitawale mimi. Ndipo nitakapokuwa kamili, Nami nitakuwa safi, sina kosa lililo kubwa.


Ampigaye baba yake au mama yake, sharti atauawa.


Aliyelemewa na damu ya mtu Atalikimbilia shimo; wala mtu asimzuie.


Lakini kama alimpiga kwa chombo cha chuma, akafa, ni mwuaji huyo; mwuaji hakika yake atauawa.


Hata ingawa niliwaambia, hamkunisikiza, bali mliasi amri ya Bwana, makajiamini na kulewa mlimani.


Atakaponena nabii kwa jina la BWANA, lisifuate jambo lile wala kutimia, hilo ndilo neno asilolinena BWANA; kwa kujikinai amelinena huyo nabii, usimwogope.


Na alaaniwe ampigaye mwenzake kwa siri. Na watu wote waseme Amina.


Maana, kama tukifanya dhambi kusudi baada ya kuupokea ujuzi wa ile kweli, haibaki tena dhabihu kwa ajili ya dhambi;


na hasa wale waufuatao mwili katika tamaa ya mambo machafu, na kudharau mamlaka.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo