Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Kumbukumbu la Torati 33:25 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

25 Makomeo yako yatakuwa ya chuma na shaba; Na kadiri ya siku zako ndivyo zitakavyokuwa nguvu zako.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

25 Miji yako ni ngome za chuma na shaba. Usalama wako utadumu maisha yako yote!”

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

25 Miji yako ni ngome za chuma na shaba. Usalama wako utadumu maisha yako yote!”

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

25 Miji yako ni ngome za chuma na shaba. Usalama wako utadumu maisha yako yote!”

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

25 Makomeo ya malango yako yawe chuma na shaba, nazo nguvu zako zitakuwa sawa na siku zako.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

25 Makomeo ya malango yako yawe chuma na shaba, nazo nguvu zako zitakuwa sawa na siku zako.

Tazama sura Nakili




Kumbukumbu la Torati 33:25
18 Marejeleo ya Msalaba  

Asheri, chakula chake kitakuwa kinono, Naye atatoa tunu za kifalme.


Kwa maana macho ya BWANA hukimbia kimbia duniani kote, ili ajionesha kuwa mwenye nguvu kwa ajili ya hao, waliokamilika moyo kuelekea kwake. Kwa hayo umetenda upumbavu; kwani tangu sasa utakuwa na vita.


Siku ile niliyokuita uliniitikia, Ukanifariji nafsi kwa kunitia nguvu.


Maana amevikaza vipingo vya malango yako, Amewabariki wanao ndani yako.


Huwapa nguvu wazimiao, humwongezea nguvu yeye asiyekuwa na uwezo.


bali wao wamngojeao BWANA watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa kama tai; watakimbia, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia.


usiogope, kwa maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia, naam, nitakushika kwa mkono wa kulia wa haki yangu.


Lakini baba aliwaambia watumwa wake, Lileteni upesi vazi lililo bora, mkamvike; mtieni na pete kidoleni, na viatu miguuni;


Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu; ila Mungu ni mwaminifu; ambaye hatawaacha mjaribiwe kupita muwezavyo; lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea, ili muweze kustahimili.


Hatimaye, mzidi kuwa hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu zake.


na kama viatu vilivyofungiwa miguuni mwenu muwe tayari kutangaza Injili ya amani;


Kwa maana si jambo lisilofaa kwenu; maana, ni maisha yenu, na kwa jambo hili mtazifanya siku zenu kuwa nyingi juu ya nchi mwivukiayo Yordani kuimiliki.


Basi, zishike sheria zake, na amri zake, ninazokuamuru leo, upate kufanikiwa, wewe na watoto wako baada yako, na siku zako ziwe nyingi katika nchi ile akupayo BWANA, Mungu wako, milele.


nchi utakayokula mikate humo, pasina shida, hutapungukiwa na kitu ndani yake; nchi ambayo mawe yake ni chuma, na milima yake mnaweza kuchimba shamba.


Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.


mkiwezeshwa kwa uwezo wote, kwa kadiri ya nguvu ya utukufu wake, mpate kuwa na subira ya kila namna na uvumilivu pamoja na furaha;


Hata sasa mimi nina nguvu zangu hivi leo kama nilivyokuwa siku hiyo Musa aliyonituma; kama nguvu zangu zilivyokuwa wakati huo, na nguvu zangu ndivyo zilivyo sasa, kwa vita na kwa kwenda na kurudi.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo