Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Isaya 43:21 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

21 watu wale niliojiumbia nafsi yangu, ili wazitangaze sifa zangu.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

21 watu niliowaumba kwa ajili yangu mwenyewe, ili wazitangaze sifa zangu!’

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

21 watu niliowaumba kwa ajili yangu mwenyewe, ili wazitangaze sifa zangu!’

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

21 watu niliowaumba kwa ajili yangu mwenyewe, ili wazitangaze sifa zangu!’

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

21 watu wale niliowaumba kwa ajili yangu, ili wapate kutangaza sifa zangu.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

21 watu wale niliowaumba kwa ajili yangu, ili wapate kutangaza sifa zangu.

Tazama sura Nakili




Isaya 43:21
22 Marejeleo ya Msalaba  

Kizazi kitakachokuja kitaandikiwa hayo, Na watu watakaoumbwa watamsifu BWANA.


Maana ametazama toka patakatifu pake pa juu, Toka mbinguni BWANA ameiangalia nchi,


Bali jueni ya kuwa BWANA amejiteulia mtauwa; BWANA husikia nimwitapo.


Na sisi tulio watu wako, Na kondoo za malisho yako, Tutakushukuru milele; Tutazisimulia sifa zako kizazi hadi kizazi.


BWANA amefanya kila kitu kwa kusudi lake; Naam, hata wabaya kwa siku ya ubaya.


Na wamtukuze BWANA, Na kutangaza sifa zake visiwani.


Lakini sasa, BWANA aliyekuhuluku, Ee Yakobo, yeye aliyekuumba, Ee Israeli, asema hivi, Usiogope, maana nimekukomboa; nimekuita kwa jina lako, wewe u wangu.


Maana Bwana MUNGU atanisaidia; kwa sababu hiyo sikutahayari, kwa sababu hiyo nimekaza uso wangu kama jiwe, nami najua ya kuwa sitaona haya.


Watu wako nao watakuwa wenye haki wote, Nao watairithi nchi milele; Wao ni chipukizi nililolipanda mimi mwenyewe, Kazi ya mikono yangu mwenyewe, Ili mimi nitukuzwe.


kuwaagizia hao waliao katika Sayuni, wapewe taji la maua badala ya majivu, mafuta ya furaha badala ya maombolezo, vazi la sifa badala ya roho nzito; wapate kuitwa miti ya haki, iliyopandwa na BWANA, ili atukuzwe.


Maana kama vile mshipi unavyoshikamana na kiuno cha mtu, ndivyo nilivyowashikamanisha nami nyumba yote ya Israeli; na nyumba yote ya Yuda, asema BWANA; wapate kuwa watu kwangu mimi, na jina, na sifa, na utukufu; lakini hawakutaka kusikia.


Na mji huu utakuwa kwangu jina la furaha, na sifa na utukufu, mbele ya mataifa yote ya dunia, watakaosikia habari ya mema yote niwatendeayo, nao wataogopa na kutetemeka, kwa sababu ya mema yote na amani nitakaoupatia mji huo.


Nao watakuwa wangu, asema BWANA wa majeshi, katika siku ile niifanyayo; naam, watakuwa hazina yangu hasa; nami nitawaachilia, kama vile mtu amwachiliavyo mwanawe mwenyewe amtumikiaye.


Basi, mlapo, au mnywapo, au mtendapo neno lolote, fanyeni yote kwa utukufu wa Mungu.


naam, atukuzwe katika kanisa na katika Kristo Yesu hata vizazi vyote vya milele na milele. Amina.


Kwa kuwa katika yeye vitu vyote viliumbwa, vilivyo mbinguni na vilivyo juu ya nchi, vinavyoonekana na visivyoonekana; ikiwa ni vitu vya enzi, au milki, au enzi, au mamlaka; vitu vyote viliumbwa kwa njia yake, na kwa ajili yake.


ambaye alijitoa nafsi yake kwa ajili yetu, ili atukomboe na maasi yote, na kujisafishia watu wake mwenyewe walio na bidii katika matendo mema.


Basi, kwa njia yake yeye, na tumpe Mungu dhabihu ya sifa daima, yaani, tunda la midomo iliungamalo jina lake.


Bali ninyi ni uzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili zake yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu;


Tufuate:

Matangazo


Matangazo