Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Isaya 35:5 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

5 Ndipo macho ya vipofu yatafumbuliwa, na masikio ya viziwi yatazibuliwa.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

5 Hapo vipofu wataona tena, na viziwi watasikia tena.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

5 Hapo vipofu wataona tena, na viziwi watasikia tena.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

5 Hapo vipofu wataona tena, na viziwi watasikia tena.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

5 Ndipo macho ya vipofu yatafumbuliwa na masikio ya viziwi yatazibuliwa.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

5 Ndipo macho ya vipofu yatafumbuliwa na masikio ya viziwi yatazibuliwa.

Tazama sura Nakili




Isaya 35:5
31 Marejeleo ya Msalaba  

Ndipo huyafunua masikio ya watu, Na kuyatia mhuri mafundisho yao,


BWANA huwafumbua macho waliopofuka; BWANA huwainua walioinama; BWANA huwapenda wenye haki;


BWANA akamwambia, Ni nani aliyekifanya kinywa cha mwanadamu? Au ni nani afanyaye mtu kuwa bubu au kiziwi, au mwenye kuona, au kuwa kipofu? Si mimi, BWANA?


Sikio lisikialo, na jicho lionalo, BWANA ndiye aliyeyafanya yote mawili.


Na katika siku hiyo viziwi watasikia maneno ya hicho kitabu, na macho ya vipofu yataona katika upofu na katika giza.


Nitawaleta vipofu kwa njia wasiyoijua; katika mapito wasiyoyajua nitawaongoza; nitafanya giza kuwa nuru mbele yao; na mahali palipopotoka kuwa pamenyoka. Haya nitayatenda, wala sitawaacha.


Sikilizeni, enyi viziwi; tazameni, enyi vipofu, mpate kuona.


Walete watu wasioona, japo wana macho, wasiosikia japo wana masikio.


Naam, hukusikia; naam, hukujua; naam, tokea zamani sikio lako halikuzibuka; maana nilijua ya kuwa wewe watenda kwa hila nyingi, nawe umeitwa mkosaji tangu kuzaliwa kwako;


Bwana MUNGU amenipa ulimi wa hao wafundishwao, nipate kujua jinsi ya kumtegemeza kwa maneno yeye aliyechoka, huniamsha asubuhi baada ya asubuhi; huniamsha, sikio langu lipate kusikia kama watu wafundishwao.


Bwana MUNGU amenizibua sikio langu, wala sikuwa mkaidi, wala sikurudi nyuma.


Niseme na nani na kushuhudia, wapate kusikia? Tazama, sikio lao halikutahiriwa, wala hawawezi kusikiliza; tazama, neno la BWANA limekuwa matukano kwao; hawalifurahii.


Wakati ule akaletewa mtu mwenye pepo, kipofu, naye ni bubu; akamponya, hata yule bubu akanena na kuona.


Na vipofu na viwete wakamwendea mle hekaluni, akawaponya.


Roho wa Bwana yu juu yangu, Kwa maana amenitia mafuta kuwahubiria maskini Habari Njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao, Na vipofu kupata kuona tena, Kuwaacha huru waliosetwa,


Bali wengine wao wakasema, Je! Huyu aliyemfumbua macho yule kipofu, hakuweza kumfanya na huyu asife?


Yesu akasema, Mimi nimekuja ulimwenguni humu kwa hukumu, ili wao wasioona waone, nao wanaoona wawe vipofu.


uwafumbue macho yao, na kuwageuza waiache giza na kuielekea nuru, waziache na nguvu za Shetani na kumwelekea Mungu; kisha wapate msamaha wa dhambi zao, na urithi miongoni mwao waliotakaswa kwa imani iliyo kwangu mimi.


Hivyo husema, Amka, wewe usinziaye, Ufufuke katika wafu, Na Kristo atakuangaza.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo