Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Isaya 33:13 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

13 Sikieni, ninyi mlio mbali, niliyoyatenda; na ninyi mlio karibu, kirini uwezo wangu.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

13 Sikilizeni mambo mliyofanya enyi mlio mbali, nanyi mlio karibu kirini uwezo wangu.”

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

13 Sikilizeni mambo mliyofanya enyi mlio mbali, nanyi mlio karibu kirini uwezo wangu.”

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

13 Sikilizeni mambo mliyofanya enyi mlio mbali, nanyi mlio karibu kirini uwezo wangu.”

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

13 Ninyi mlio mbali sana, sikieni lile nililofanya; ninyi mlio karibu, tambueni uweza wangu!

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

13 Ninyi mlio mbali sana, sikieni lile nililofanya; ninyi mlio karibu, tambueni uweza wangu!

Tazama sura Nakili




Isaya 33:13
21 Marejeleo ya Msalaba  

Naye amewainulia watu wake pembe, Sifa za watauwa wake wote; Wana wa Israeli, watu walio karibu naye. Haleluya.


Kama lilivyo jina lako, Ee Mungu, Ndivyo na sifa yako hadi miisho ya dunia. Mkono wako wa kulia umejaa haki;


Sayuni imesikia na kufurahi, Binti za Yuda walishangilia, Kwa sababu ya hukumu zako, Ee BWANA.


Makabila ya watu wamesikia, wanatetemeka, Wakazi wa Ufilisti uchungu umewashika.


Enyi watu mkaao katika ulimwengu wote, na wenyeji wa dunia, bendera ikiinuliwa milimani, angalieni; na wakipiga tarumbeta, sikieni.


Basi sasa, BWANA, Mungu wetu, utuokoe kutoka kwa mkono wake, falme zote za dunia zipate kujua ya kuwa wewe ndiwe BWANA, wewe peke yako.


Nisikilizeni, enyi visiwa; tegeni masikio yenu, enyi makabila ya watu mlio mbali sana; BWANA ameniita tangu tumboni; toka tumbo la mama yangu amenitaja jina langu.


BWANA ameweka wazi mkono wake mtakatifu Machoni pa mataifa yote; Na ncha zote za dunia Zitauona wokovu wa Mungu wetu.


Mimi nayaumba matunda ya midomo; Amani, amani, kwake yeye aliye mbali, na kwake yeye aliye karibu; asema BWANA; nami nitamponya.


Na maamiri, wasimamizi, watawala, na mahakimu, waliokuwa wamekusanyika pamoja, wakawaona watu hao, ya kuwa ule moto ulikuwa hauna nguvu juu ya miili yao, wala nywele za vichwa vyao hazikuteketea, wala suruali zao hazikubadilika, wala harufu ya moto haikuwapata hata kidogo.


Siku hii ya leo BWANA atakuua mkononi mwangu, nami nitakupiga, na kukuondolea kichwa chako, nami leo nitawapa ndege wa angani na wanyama wa nchi mizoga ya majeshi ya Wafilisti, ili kwamba dunia nzima wajue ya kuwa yuko Mungu katika Israeli.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo