Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Isaya 31:9 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

9 Na mwamba wake utatoweka kwa sababu ya hofu, nao wakuu wake wataionea bendera hofu kuu, asema BWANA, ambaye moto wake u katika Sayuni, na tanuri yake katika Yerusalemu.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

9 Mfalme wao atatoroka kwa hofu, na maofisa wao wataiacha bendera yao kwa woga. Hayo ameyatamka Mwenyezi-Mungu ambaye moto wake umo mjini Siyoni, naam, tanuri lake limo mjini Yerusalemu.”

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

9 Mfalme wao atatoroka kwa hofu, na maofisa wao wataiacha bendera yao kwa woga. Hayo ameyatamka Mwenyezi-Mungu ambaye moto wake umo mjini Siyoni, naam, tanuri lake limo mjini Yerusalemu.”

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

9 Mfalme wao atatoroka kwa hofu, na maofisa wao wataiacha bendera yao kwa woga. Hayo ameyatamka Mwenyezi-Mungu ambaye moto wake umo mjini Siyoni, naam, tanuri lake limo mjini Yerusalemu.”

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

9 Ngome zao zitaanguka kwa sababu ya hofu; kwa kuona bendera ya vita, majemadari wao watashikwa na hofu ya ghafula,” asema Mwenyezi Mungu, ambaye moto wake uko Sayuni, nalo tanuru lake liko Yerusalemu.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

9 Ngome zao zitaanguka kwa sababu ya hofu; kwa kuona bendera ya vita, majemadari wao watashikwa na hofu ya ghafula,” asema bwana, ambaye moto wake uko Sayuni, nayo tanuru yake iko Yerusalemu.

Tazama sura Nakili




Isaya 31:9
20 Marejeleo ya Msalaba  

Kwa hiyo Bwana, BWANA wa majeshi, atatuma maradhi ya kukondesha kwa wapiganaji walionenepa; na badala ya utukufu wake kutawashwa kuteketea kama kuteketea kwa moto.


Na mwanga wa Israeli utakuwa ni moto, na Mtakatifu wake atakuwa muali wa moto; nao utateketeza na kula mbigili zake na miiba yake kwa siku moja.


Na itakuwa katika siku hiyo, shina la Yese lisimamalo kuwa ishara kwa makabila ya watu, yeye ndiye ambaye mataifa watamtafuta; na mahali pake pa kupumzikia patakuwa na utukufu.


Haya! Juu ya mlima usio na miti inueni bendera, wapazieni sauti zenu, wapungieni mkono, kwamba waingie katika malango ya wakuu.


Mataifa wananguruma kama ngurumo ya maji mengi; Lakini atawakemea, nao watakimbia mbali sana, Watafukuzwa kama makapi milimani mbele ya upepo, Na kama mavumbi vuruvuru mbele ya tufani.


Enyi watu mkaao katika ulimwengu wote, na wenyeji wa dunia, bendera ikiinuliwa milimani, angalieni; na wakipiga tarumbeta, sikieni.


Siku ile wimbo huu utaimbwa katika nchi ya Yuda; Sisi tunao mji ulio na nguvu; Ataamuru wokovu kuwa kuta na maboma.


Je! Amempiga kama hilo pigo la hao waliompiga, au ameuawa kama walivyouawa wao waliouawa na yeye?


Naye atajiliwa na BWANA wa majeshi kwa ngurumo, na tetemeko la nchi, na sauti kuu, na chamchela, na tufani, na mwali wa moto uteketezao.


Maana Tofethi imewekwa tayari tokea zamani, naam, imewekwa tayari kwa mfalme huyo; ameifanya kubwa, inakwenda chini sana; tanuri yake ni moto na kuni nyingi; pumzi ya BWANA, kama mto wa kiberiti, huiwasha.


Basi Senakeribu, mfalme wa Ashuru akaenda zake, akarudi Ninawi, akakaa huko.


hapo Bwana atakapokuwa ameuosha uchafu wa hao binti za Sayuni na kuisafisha damu ya Yerusalemu kati yake, kwa roho ya hukumu na kwa roho ya kuteketeza.


Naye atawatolea ishara mataifa toka mbali, Naye atawapigia miruzi tokea mwisho wa nchi; Na tazama, watakuja mbio mbio upesi sana.


Maana BWANA atakuja na moto, na magari yake ya vita kama upepo wa kisulisuli; ili atoe malipo ya ghadhabu yake kwa moto uwakao, na maonyo yake kwa miali ya moto.


Moto utatunzwa uwake juu ya madhabahu daima; usizimike.


Kwa maana mimi, asema BWANA, nitakuwa ukuta wa moto kuuzunguka pande zote, nami nitakuwa huo utukufu ndani yake.


Kwa maana, angalieni, siku ile inakuja, inawaka kama tanuri; na watu wote wenye kiburi, nao wote watendao uovu, watakuwa makapi; na siku ile inayokuja itawateketeza, asema BWANA wa majeshi; hata haitawaachia shina wala tawi.


Maana, Mwamba wao si kama Mwamba wetu, Hata adui zetu wenyewe ndivyo wahukumuvyo.


Naye atasema, Iko wapi miungu yao, Mwamba ule walioutumaini;


Tufuate:

Matangazo


Matangazo