Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Hesabu 21:29 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

29 Ole wako Moabu! Umeangamia, enyi watu wa Kemoshi; Amewatoa wanawe kuwa wakimbizi, Na binti zake waende utumwani, Wamwendee Sihoni mfalme wa Waamori.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

29 Ole wenu watu wa Moabu! Mmeangamizwa, enyi watu wa mungu Kemoshi! Umewafanya watoto wenu wa kiume kuwa wakimbizi, binti zako umewaacha wachukuliwe mateka mpaka kwa Sihoni, mfalme wa Amori.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

29 Ole wenu watu wa Moabu! Mmeangamizwa, enyi watu wa mungu Kemoshi! Umewafanya watoto wenu wa kiume kuwa wakimbizi, binti zako umewaacha wachukuliwe mateka mpaka kwa Sihoni, mfalme wa Amori.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

29 Ole wenu watu wa Moabu! Mmeangamizwa, enyi watu wa mungu Kemoshi! Umewafanya watoto wenu wa kiume kuwa wakimbizi, binti zako umewaacha wachukuliwe mateka mpaka kwa Sihoni, mfalme wa Amori.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

29 Ole wako, ee Moabu! Umeharibiwa, enyi watu wa Kemoshi! Amewatoa wanawe kuwa wakimbizi, na binti zake kama mateka kwa Mfalme Sihoni wa Waamori.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

29 Ole wako, ee Moabu! Umeharibiwa, enyi watu wa Kemoshi! Amewatoa wanawe kuwa wakimbizi, na binti zake kama mateka kwa Mfalme Sihoni wa Waamori.

Tazama sura Nakili




Hesabu 21:29
12 Marejeleo ya Msalaba  

kwa sababu wameniacha mimi wakaabudu Ashtorethi, mungu mke wa Wasidoni, na Kemoshi, mungu wa Wamoabi, na Milkomu, mungu wa wana wa Amoni wala hawakuenda katika njia zangu, kutenda mema machoni pangu, kuzishika sheria zangu na hukumu zangu, kama Daudi baba yake.


Sulemani akamjengea Kemoshi, chukizo la Wamoabi, mahali pa juu, katika mlima uliokabili Yerusalemu, na Moleki, chukizo la wana wa Amoni.


Na mahali pa juu palipokuwapo mbele ya Yerusalemu, palipokuwa upande wa kulia wa mlima wa uharibifu, alipopajenga Sulemani, mfalme wa Israeli, kwa Ashtorethi, chukizo la Wasidoni, na Kemoshi, chukizo la Moabu, na Milkomu, chukizo la wana wa Amoni, mfalme akapanajisi.


Moyo wangu unamlilia Moabu; wakuu wake wanakimbilia Soari kama ndama wa miaka mitatu; kwa maana wanapanda mbavu za Luhithi wakilia; maana katika njia iendayo hata Horonaimu wanatoa kilio cha maangamizi.


Na binti za Moabu watakuwa kama ndege warukao huku na huko, kama kiota cha ndege waliotiwa hofu, kwenye vivuko vya Arnoni.


Na Moabu ataona haya kwa ajili ya Kemoshi, kama nyumba ya Israeli ilivyoona haya kwa ajili ya Betheli, tegemeo lao.


Wamekimbia, wasio na nguvu Wanasimama chini ya kivuli cha Heshboni; Ila moto umetoka katika Heshboni, Na muali wa moto toka kati ya Sihoni Nao umekula pembe ya Moabu, Na utosi wa kichwa wa watu wapigao kelele.


Ole wako! Ee Moabu, Watu wa Kemoshi wamepotea; Maana wana wako wamechukuliwa mateka, Na binti zako wamekwenda utumwani.


Maana, kwa kuwa umeyatumainia matendo yako, na hazina zako, wewe nawe utatwaliwa; na Kemoshi atatoka aende katika uhamisho, makuhani wake na wakuu wake pamoja.


Namwona, lakini si sasa; Namtazama, lakini si karibu; Nyota itatokea katika Yakobo Na fimbo ya enzi itainuka katika Israeli; Nayo itazipigapiga pembe za Moabu, Na kuwavunjavunja wana wote wa ghasia.


Je! Wewe hutakitamalaki hicho ambacho huyo Kemoshi mungu wako akupa kukitamalaki? Kadhalika si sisi ndio watu wa kutamalaki vyote ambavyo BWANA, Mungu wetu ametwaa kwa manufaa yetu?


Tufuate:

Matangazo


Matangazo