Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Ezekieli 48:18 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

18 Na mabaki ya urefu wake yaelekeayo matoleo matakatifu, upande wa mashariki yatakuwa mianzi elfu kumi, na upande wa magharibi mianzi elfu kumi; nayo yatakuwa sawasawa na matoleo matakatifu; na mazao yake yatakuwa ni chakula cha watu wafanyao kazi humo mjini.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

18 Eneo ambalo litabaki baada ya kujengwa hekalu, kusini mwa mji, kilomita 5 kwa kilomita 2.5, upande wa mashariki, na kilomita 5 kwa kilomita 2.5 upande wa magharibi, litakuwa eneo la wakulima kwa wakazi wa mji.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

18 Eneo ambalo litabaki baada ya kujengwa hekalu, kusini mwa mji, kilomita 5 kwa kilomita 2.5, upande wa mashariki, na kilomita 5 kwa kilomita 2.5 upande wa magharibi, litakuwa eneo la wakulima kwa wakazi wa mji.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

18 Eneo ambalo litabaki baada ya kujengwa hekalu, kusini mwa mji, kilomita 5 kwa kilomita 2.5, upande wa mashariki, na kilomita 5 kwa kilomita 2.5 upande wa magharibi, litakuwa eneo la wakulima kwa wakazi wa mji.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

18 Eneo linalobaki, linalopakana na sehemu takatifu likiwa na urefu sawa nalo, litakuwa dhiraa elfu kumi upande wa mashariki, na dhiraa elfu kumi upande wa magharibi. Mazao yake yatawapa watumishi wa mji chakula.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

18 Eneo linalobaki, linalopakana na sehemu takatifu likiwa na urefu sawa nalo, litakuwa dhiraa 10,000 upande wa mashariki na dhiraa 10,000 upande wa magharibi. Mazao yake yatawapa watumishi wa mji chakula.

Tazama sura Nakili




Ezekieli 48:18
6 Marejeleo ya Msalaba  

Nanyi mtaiandika milki ya mji, upana wake elfu tano, na urefu wake elfu ishirini na tano, kandokando ya mahali palipotolewa, iwe sehemu takatifu; nayo itakuwa ya nyumba yote ya Israeli.


Nao mji utakuwa na malisho; upande wa kaskazini mianzi mia mbili na hamsini, na upande wa kusini mianzi mia mbili na hamsini, na upande wa mashariki mianzi mia mbili na hamsini, na upande wa magharibi mianzi mia mbili na hamsini.


Na hao wafanyao kazi mjini, wa kabila zote za Israeli, watailima nchi hiyo.


Siku iyo hiyo Yoshua akawafanya kuwa ni wenye kupasua kuni, na wenye kuteka maji, kwa ajili ya mkutano, na kwa ajili ya madhabahu ya BWANA, hata siku hii ya leo, katika mahali hapo atakapopachagua.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo