Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Ezekieli 47:6 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

6 Akaniambia, Mwanadamu, je! Umeona haya? Kisha akanichukua akanirudisha mpaka ukingo wa mto.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

6 Yule mtu akaniambia, “Wewe mtu! Zingatia mambo hayo yote kwa makini.” Kisha, akanirudisha mpaka ukingo wa mto.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

6 Yule mtu akaniambia, “Wewe mtu! Zingatia mambo hayo yote kwa makini.” Kisha, akanirudisha mpaka ukingo wa mto.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

6 Yule mtu akaniambia, “Wewe mtu! Zingatia mambo hayo yote kwa makini.” Kisha, akanirudisha mpaka ukingo wa mto.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

6 Akaniuliza, “Je, mwanadamu, unaona hili?” Kisha akanirudisha kwenye ukingo wa huo mto.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

6 Akaniuliza, “Je, mwanadamu, unaona hili?” Kisha akanirudisha mpaka kwenye ukingo wa huo mto.

Tazama sura Nakili




Ezekieli 47:6
8 Marejeleo ya Msalaba  

Mtu yule akaniambia, Mwanadamu, tazama kwa macho yako, sikia kwa masikio yako, ukaweke moyoni mwako, yote nitakayokuonesha; maana umeletwa hapa kusudi nikuoneshe haya; tangaza habari ya yote utakayoyaona kwa nyumba ya Israeli.


BWANA akaniambia, Mwanadamu, weka moyoni mwako, ukatazame kwa macho yako, ukasikie kwa masikio yako, maneno yote nitakayokuambia, katika habari ya kawaida zote za nyumba ya BWANA, na ya amri zake zote; nawe weka moyoni mwako maingilio ya nyumba, pamoja na matokeo yote ya mahali patakatifu.


Basi, akaniambia, Umeyaona haya, Ee mwanadamu? Je! Ni jambo dogo sana kwa nyumba ya Yuda, wayafanye machukizo wanayoyafanya hapa? Kwa maana wameijaza nchi hii udhalimu, tena wamerejea nyuma ili kunikasirisha; na, tazama, wanaliweka tawi puani.


Akaniambia, Mwanadamu, je! Unayaona wanayoyafanya, yaani, haya machukizo makubwa wanayoyafanya nyumba ya Israeli hapa, ili niende zangu mbali na patakatifu pangu? Lakini utaona tena machukizo makubwa mengine.


Akaniuliza, Unaona nini? Nikasema, Nimeona, na tazama, kinara cha taa cha dhahabu tupu, nacho kina bakuli juu yake, na taa zake saba juu yake; tena iko mirija saba ya kuleta mafuta, kwa taa zote zilizo juu yake;


Akaniuliza, Unaona nini? Nikajibu, Naona gombo la kitabu lirukalo; na urefu wake ni dhiraa ishirini, na upana wake dhiraa kumi.


Yesu aliwauliza, Mmeyafahamu hayo yote? Wakamwambia, Naam.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo