Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Ezekieli 35:2 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

2 Mwanadamu, kaza uso wako juu ya mlima Seiri, ukatabiri juu yake,

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

2 “Wewe mtu! Ugeukie mlima Seiri, utoe unabii juu ya wakazi wake.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

2 “Wewe mtu! Ugeukie mlima Seiri, utoe unabii juu ya wakazi wake.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

2 “Wewe mtu! Ugeukie mlima Seiri, utoe unabii juu ya wakazi wake.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

2 “Mwanadamu, elekeza uso wako juu ya Mlima Seiri, utabiri dhidi yake

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

2 “Mwanadamu, elekeza uso wako juu ya mlima Seiri, utabiri dhidi yake

Tazama sura Nakili




Ezekieli 35:2
28 Marejeleo ya Msalaba  

Basi, Yakobo akapeleka wajumbe mbele yake kwenda kwa Esau nduguye mpaka nchi ya Seiri katika nyika ya Edomu.


Na sasa, tazama, wana wa Amoni, na Moabu, na wa mlima Seiri, ambao hukuwaacha Israeli waingie katika nchi yao, walipotoka nchi ya Misri; lakini wakawageukia mbali, wasiwaharibu;


Ee BWANA, uwakumbuke wana wa Edomu, Siku ile Yerusalemu ilipotekwa. Kwa namna walivyosema, Bomoeni! Bomoeni hata misingini!


Maana Bwana MUNGU atanisaidia; kwa sababu hiyo sikutahayari, kwa sababu hiyo nimekaza uso wangu kama jiwe, nami najua ya kuwa sitaona haya.


Mwanadamu, uelekeze uso wako kusini, ukadondoze neno lako upande wa kusini, ukatabiri juu ya msitu wa uwanda wa Negebu,


Mwanadamu, uelekeze uso wako Yerusalemu, ukadondoze neno lako upande wa mahali patakatifu, ukatabiri juu ya nchi ya Israeli;


Mwanadamu, uwaelekezee wana wa Amoni uso wako, ukatabiri juu yao.


Bwana MUNGU asema hivi; Kwa sababu Moabu na Seiri husema, Tazama, nyumba ya Israeli ni sawasawa na mataifa yote;


Edomu yuko huko, wafalme wake, na wakuu wake wote, ambao katika uwezo wao wamelazwa pamoja nao waliouawa kwa upanga; watalala pamoja na hao wasiotahiriwa, na pamoja na hao washukao shimoni.


Tena neno la BWANA likanijia, kusema,


basi Bwana MUNGU asema hivi; Hakika kwa moto wa wivu wangu nimenena juu ya mabaki ya mataifa, na juu ya Edomu yote, waliojiandalia nchi yangu kuwa milki yao, kwa furaha ya mioyo yao yote, kwa ujeuri wa roho zao, wakatwaa nchi yangu kuwa milki yao, kwa sababu ya malisho yake, ili kuipora;


Mwanadamu, uelekeze uso wako uitazame milima ya Israeli, ukaitabirie,


Maono yake Obadia. Ndivyo asemavyo Bwana MUNGU juu ya Edomu; Tumepata habari kwa BWANA, Na mjumbe ametumwa kati ya mataifa, Akisema, Haya, inukeni ninyi; Na tuinuke tupigane naye.


pia na kwa ajili yangu mimi, nipewe usemi kwa kufumbua kinywa changu, ili niihubiri kwa ujasiri ile siri ya Injili;


msipigane nao; kwa kuwa sitawapa sehemu ya nchi yao kamwe, hata kiasi cha kukanyaga wayo wa mguu; kwa kuwa nimempa Esau milima ya Seiri kuwa milki yake.


Kisha nikampa huyo Isaka, Yakobo na Esau; nami nikampa Esau mlima Seiri aumiliki; Yakobo na watoto wake wakashuka Misri.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo