Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Ezekieli 23:26 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

26 Pia watakuvua nguo zako, na kukunyang'anya johari zako uzuri.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

26 Watakuvua mavazi yako na kukunyanganya johari zako nzuri.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

26 Watakuvua mavazi yako na kukunyanganya johari zako nzuri.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

26 Watakuvua mavazi yako na kukunyang'anya johari zako nzuri.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

26 Watakuvua nguo zako pia, na kuchukua mapambo yako yaliyotengenezwa kwa vito na dhahabu.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

26 Watakuvua pia nguo zako na kuchukua mapambo yako yaliyotengenezwa kwa vito na dhahabu.

Tazama sura Nakili




Ezekieli 23:26
13 Marejeleo ya Msalaba  

Akatoa huko hazina zote za nyumba ya BWANA, na hazina za nyumba ya mfalme, akavikatakata vyombo vyote vya dhahabu ambavyo Sulemani, mfalme wa Israeli, alivitengeneza katika hekalu la BWANA, kama BWANA alivyosema.


Tazama, siku zinakuja, ambazo vitu vyote vilivyomo nyumbani mwako, na hivyo vilivyowekwa akiba na baba zako hata leo, vitachukuliwa mpaka Babeli; hapana kitu chochote kitakachosalia; asema BWANA.


Nawe ukisema moyoni mwako, Mbona mambo haya yamenipata mimi? Ni kwa sababu ya wingi wa uovu wako, marinda yako yamefunuliwa, na visigino vya miguu yako vimeumia.


Ukatwaa baadhi ya mavazi yako, ukajifanyia mahali palipoinuka, palipopambwa kwa rangi mbalimbali, ukafanya mambo ya kikahaba juu yake; mambo kama hayo hayatakuja wala hayatakuwako.


basi, tazama, nitawakusanya wapenzi wako wote ambao umejifurahisha pamoja nao, nao wote uliowapenda, pamoja na watu wote uliowachukia; naam, nitawakusanya juu yako pande zote, na kuwafunulia uchi wako, wapate kuuona uchi wako wote.


Tena nitakutia katika mikono yao, nao watapaangusha mahali pako pakuu, na kupabomoa mahali pako palipoinuka, nao watakuvua nguo zako, na kutwaa vyombo vyako vya uzuri, nao watakuacha uchi, bila mavazi.


nao watakutenda mambo kwa chuki, watakunyang'anya matunda yote ya kazi yako, watakuacha uchi, huna nguo na aibu ya mambo yako ya kikahaba itafunuliwa, uasherati wako na uzinzi wako.


nisije nikamvua nguo zake akawa uchi, nikamweka katika hali aliyokuwa nayo siku ya kuzaliwa kwake, na kumfanya kama jangwa, na kumweka kama nchi kame, na kumwua kwa kiu;


Na zile pembe kumi ulizoziona, na huyo mnyama, hao watamchukia yule kahaba, nao watamfanya kuwa mkiwa na uchi, watamla nyama yake, watamteketeza kabisa kwa moto.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo