Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Ezekieli 16:32 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

32 Mke wa mtu, aziniye! Akaribishaye wageni badala ya mumewe!

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

32 Ulikuwa mke mzinzi akaribishaye wageni badala ya mumewe.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

32 Ulikuwa mke mzinzi akaribishaye wageni badala ya mumewe.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

32 Ulikuwa mke mzinzi akaribishaye wageni badala ya mumewe.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

32 “ ‘Wewe mke mzinzi! Unapenda wageni, kuliko mume wako mwenyewe.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

32 “ ‘Wewe mke mzinzi! Unapenda wageni, kuliko mume wako mwenyewe.

Tazama sura Nakili




Ezekieli 16:32
15 Marejeleo ya Msalaba  

Maana mume wangu hayumo nyumbani, Amekwenda safari ya mbali;


Zuia mguu wako usikose kiatu, na koo yako isiwe na kiu; lakini wewe ulisema, Hakuna matumaini kabisa; la, maana nimewapenda wageni, nami nitawafuata.


Lakini wako wapi miungu yako ulioifanya? Na wasimame hao, kama wakiweza kukuokoa wakati wa taabu yako; kwa maana hesabu ya miungu yako ni sawa na hesabu ya miji yako, Ee Yuda.


Watu husema, Mtu akimwacha mkewe, naye akienda zake, akawa mke wa mtu mwingine, je! Mtu huyo atamrudia tena? Je! Nchi hiyo haitatiwa unajisi? Lakini wewe umefanya mambo ya ukahaba na wapenzi wengi; nawe, je! Utanirudia mimi? Asema BWANA.


Bali, kama vile mke amwachavyo mumewe kwa hiana, ndivyo mlivyonitenda mimi kwa hiana, Ee nyumba ya Israeli, asema BWANA.


apendaye kutawala watu; kwa kuwa wajijengea mahali pako pakuu penye kichwa cha kila njia, na kufanya mahali pako palipoinuka katika kila njia kuu; lakini hukuwa kama kahaba, kwa maana ulidharau kupokea ujira.


Watu huwapa makahaba wote zawadi, bali wewe unawapa wapenzi wako wote zawadi zako, na kuwapa rushwa ili waje kwako pande zote, kwa ajili ya mambo yako ya kikahaba.


Basi, nilipopita karibu nawe, nikakutazama; tazama, wakati wako ulikuwa wakati wa upendo; nikatandika upindo wa vazi langu juu yako, nikakufunika uchi wako; naam, nilikuapia, nikafanya agano nawe, asema Bwana MUNGU, ukawa wangu.


Maana wamezini, na damu imo mikononi mwao, nao wamezini na vinyago vyao; tena wana wao walionizalia wamewapitisha katika moto ili waliwe nao.


Basi watu wenye haki watawahukumu, kwa hukumu iwapasayo wazinzi, na kwa hukumu iwapasayo wanawake wamwagao damu; kwa sababu wao ndio wazinzi, na mikononi mwao mna damu.


Msihini mama yenu, msihini; kwa maana yeye si mke wangu, wala mimi si mume wake; na aondokane na usherati wake usiwe mbele ya uso wake, na uzinzi wake usiwe kati ya matiti yake;


BWANA akaniambia, Nenda tena, mpende mwanamke apendwaye na rafiki yake, naye ni mzinzi; kama vile BWANA awapendavyo wana wa Israeli, ingawa wanaigeukia miungu mingine, na kupenda mikate ya zabibu kavu.


Enyi wazinzi, hamjui ya kwamba kuwa rafiki wa dunia ni kuwa adui wa Mungu? Basi kila atakaye kuwa rafiki wa dunia hujifanya kuwa adui wa Mungu.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo