Kitabu hiki si kilichoandikwa kwa uvuvio wa Mungu, na si sehemu ya kanoni ya Kikristo wala Tanaki ya Kiyahudi. Kinaonyeshwa kwa madhumuni ya kihistoria na ya utafiti tu. Tazama maelezo kamili Esta G 3_1:15 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC15 Matarishi wakaondoka wakaenda haraka kwa amri ya mfalme; kukapigwa mbiu huko Shushani ngomeni. Mfalme na Hamani wakaketi ili kunywa divai; bali mji wa Shushani ukafadhaika. Tazama suraBiblia Habari Njema - BHND15 Kwa amri ya mfalme, tangazo hili lilitolewa katika mji mkuu wa Susa, nao matarishi wakalitangaza katika mikoa yote. Mfalme na Hamani walikaa wanastarehe pamoja wakati watu mjini Susa wanafadhaika. Tazama suraBiblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza15 “Baada ya kuwa mtawala wa mataifa mengi na bwana wa dunia nzima, niliamua kuwa maisha ya raia wangu lazima yawe katika amani daima. Nilitaka hilo, si kwa sababu ya majivuno yanayotokana na mamlaka yangu, bali kwa sababu daima nimekuwa nikitenda kwa busara na kuwatawala raia wangu kwa upole. Nilidhamiria kuirudisha amani na kupanga lolote linalowezekana ili kujenga ufalme uliostaarabika wenye usalama wa kusafiri, toka pembe hii hadi pembe nyingine. Tazama suraBIBLIA KISWAHILI15 Kwa kuwa nimepata kutawala mataifa mengi na kuimiliki dunia yote – wala si kama ninaufurahia huo uwezo wangu kwa kiburi, ila nia yangu ni kuyaongoza maisha yangu kwa kiasi na upole – kwa hiyo nimetaka kuthibitisha maisha ya raia wangu katika utulivu wa daima, na kuufanya ufalme wangu uwe na amani, hata mtu apite salama toka mpaka hata mpaka, na kuirudisha ile hali ya amani inayotakiwa na watu wote. Tazama suraBIBLIA Yenye Vitabu vya Deuterokanoni HABARI NJEMA15 “Baada ya kuwa mtawala wa mataifa mengi na bwana wa dunia nzima, niliamua kuwa maisha ya raia wangu lazima yawe katika amani daima. Nilitaka hilo, si kwa sababu ya majivuno yanayotokana na mamlaka yangu, bali kwa sababu daima nimekuwa nikitenda kwa busara na kuwatawala raia wangu kwa upole. Nilidhamiria kuirudisha amani na kupanga lolote linalowezekana ili kujenga ufalme uliostaarabika wenye usalama wa kusafiri, toka pembe hii hadi pembe nyingine. Tazama sura |