Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




2 Wathesalonike 1:6 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

6 Kwa kuwa ni haki mbele za Mungu kuwalipa mateso wale wawatesao ninyi;

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

6 Mungu atafanya jambo la haki: Atawalipa mateso wale wanaowatesa nyinyi

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

6 Mungu atafanya jambo la haki: Atawalipa mateso wale wanaowatesa nyinyi

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

6 Mungu atafanya jambo la haki: atawalipa mateso wale wanaowatesa nyinyi

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

6 Mungu ni mwenye haki: yeye atawalipa mateso wale wanaowatesa ninyi,

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

6 Mungu ni mwenye haki: yeye atawalipa mateso wale wawatesao ninyi

Tazama sura Nakili




2 Wathesalonike 1:6
18 Marejeleo ya Msalaba  

Lakini ukiisikiza sauti yake kweli, na kuyatenda yote ninenayo mimi; ndipo mimi nitakuwa ni adui wa adui zako, na mtesi wa hao wakutesao.


Nikasema moyoni mwangu, Mungu atawahukumu wenye haki na wasio haki; kwa kuwa kuna wakati huko kwa kila kusudi na kwa kila kazi.


Na hao wanaokuonea nitawalisha nyama yao wenyewe, nao watalewa kwa kuinywa damu yao wenyewe, kama kwa mvinyo mpya; na watu wote watajua ya kuwa mimi, BWANA, ni mwokozi wako, na Mkombozi wako ni Mwenye enzi wa Yakobo.


Waiteni wapiga mishale juu ya Babeli, Naam, wote waupindao upinde; Pangeni hema kumzunguka pande zote; Ili asiokoke hata mtu mmoja wao; Mlipeni kwa kadiri ya kazi yake; Mtendeni sawasawa na yote aliyoyatenda; Kwa sababu amefanya kiburi juu ya BWANA, Juu yake aliye Mtakatifu wa Israeli.


Kwa maana BWANA wa majeshi asema hivi, Ili nitafute utukufu amenituma kwa mataifa wale waliowateka ninyi; maana yeye awagusaye ninyi aigusa mboni ya jicho lake.


Maana adhulumuye atapata mapato ya udhalimu wake, wala hakuna upendeleo.


Maana Mungu si dhalimu hata aisahau kazi yenu, na pendo lile mlilolidhihirisha kwa jina lake, kwa kuwa mmewahudumia watakatifu, na hata hivi sasa mngali mkiwahudumia.


Na mataifa walikasirika, hasira yako nayo ikaja, na wakati ukaja wa kuhukumiwa waliokufa, na wa kuwapa thawabu yao watumishi wako manabii na watakatifu, na hao walichao jina lako, wadogo kwa wakubwa, na wa kuwaharibu hao waiharibuo nchi.


Ni nani asiyekucha, Ee Bwana, na kulitukuza jina lako? Kwa kuwa wewe peke yako u Mtakatifu; kwa maana mataifa yote watakuja na kusujudu mbele zako; kwa kuwa matendo yako ya haki yamekwisha kufunuliwa.


Furahini juu yake, enyi mbingu, na enyi watakatifu, mitume na manabii; kwa maana Mungu ametoa hukumu kwa ajili yenu juu yake.


Na ndani yake ilionekana damu ya manabii, na ya watakatifu, na ya wale wote waliouawa juu ya nchi.


kwa kuwa hukumu zake ni za kweli na haki; maana amemhukumu yule kahaba mkuu aliyeiharibu nchi kwa uasherati wake, na kuipatiliza damu ya watumwa wake mkononi mwake.


Wakalia kwa sauti kuu, wakisema, Ee Mola, Mtakatifu, na Mkweli, utakawia hadi lini kuhukumu na kuilipa damu yetu kwa hao wakaao juu ya nchi?


Tufuate:

Matangazo


Matangazo