Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




2 Wakorintho 9:6 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

6 Lakini nasema neno hili, Apandaye haba atavuna haba; apandaye kwa ukarimu atavuna kwa ukarimu.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

6 Kumbukeni: “Apandaye kidogo huvuna kidogo; apandaye kwa wingi huvuna kwa wingi.”

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

6 Kumbukeni: “Apandaye kidogo huvuna kidogo; apandaye kwa wingi huvuna kwa wingi.”

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

6 Kumbukeni: “Apandaye kidogo huvuna kidogo; apandaye kwa wingi huvuna kwa wingi.”

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

6 Kumbukeni kwamba: Yeyote apandaye haba pia atavuna haba, naye apandaye kwa ukarimu pia atavuna kwa ukarimu.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

6 Kumbukeni kwamba: Yeyote apandaye kwa uchache pia atavuna kwa uchache, naye apandaye kwa ukarimu pia atavuna kwa ukarimu.

Tazama sura Nakili




2 Wakorintho 9:6
20 Marejeleo ya Msalaba  

Mtu mwovu hupata mshahara wa udanganyifu; Apandaye haki ana thawabu ya hakika.


Amhurumiaye maskini humkopesha BWANA; Naye atamlipa kwa tendo lake jema.


Mwenye jicho la ukarimu atabarikiwa; Maana huwapa maskini chakula chake.


Tupa chakula chako juu ya maji; Maana utakiona baada ya siku nyingi.


Asubuhi panda mbegu zako, Wala jioni usiulegeze mkono wako. Kwa maana wewe hujui ni zipi zitakazofanikiwa, kama ni hii au hii, au kama zote zitafaa sawasawa.


Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa; kipimo cha kujaa na kushindiliwa, na kusukwasukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa vifuani mwenu. Kwa kuwa kipimo kile kile mpimacho ndicho mtakachopimiwa.


Basi, maana yangu ni hii, ya kwamba kila mtu wa kwenu kusema, Mimi ni wa Paulo, na, Mimi ni wa Apolo, na, Mimi ni wa Kefa, na, Mimi ni wa Kristo.


Lakini sasa Kristo amefufuka katika wafu, limbuko lao waliolala.


Lakini, ndugu, nasema hivi, muda ubakio si mwingi; basi tokea sasa wale walio na wake na wawe kama hawana;


Na yeye ampaye mbegu mwenye kupanda, na mkate uwe chakula, atawapa mbegu za kupanda na kuzizidisha, naye atayaongeza mazao ya haki yenu;


Basi niliona ya kuwa ni lazima niwaonye ndugu hawa watangulie kufika kwenu, na kutengeneza mapema karama yenu mliyoahidi tangu zamani, ili iwe tayari, na hivi iwe kama kipawa, wala si kama kitu kitolewacho kwa nguvu.


Nisemalo ni hili; agano lililothibitishwa kwanza na Mungu, torati iliyotokea miaka mia nne na thelathini baadaye hailitangui, hata kuibatilisha ile ahadi.


Basi nasema, Nendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili.


Basi nasema neno hili, tena nashuhudia katika Bwana, tangu sasa msiende kama Mataifa waenendavyo, katika ubatili wa nia zao;


Nasema neno hili, mtu asije akawadanganya kwa maneno ya kuwashawishi.


Maana Mungu si dhalimu hata aisahau kazi yenu, na pendo lile mlilolidhihirisha kwa jina lake, kwa kuwa mmewahudumia watakatifu, na hata hivi sasa mngali mkiwahudumia.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo