Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




2 Wafalme 19:23 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

23 Kwa vinywa vya wajumbe wako umemshutumu Bwana, ukasema, Kwa wingi wa magari yangu nimepanda juu ya vilele vya milima, mpaka mahali pa ndani pa Lebanoni. Nami nitaikata mierezi yake mirefu, na misonobari yake mizuri; nami nitaingia ndani ya makazi yake yaliyo mbali sana, na msitu wa shamba lake lizaalo sana.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

23 Kwa kuwatuma wajumbe wako umemkashifu Bwana, wewe umesema, “Kwa magari yangu mengi ya vita, nimekwea vilele vya milima mpaka kilele cha Lebanoni. Nimekata mierezi yake mirefu, na misonobari mizurimizuri; nimeingia mpaka ndani yake na ndani ya misitu yake mikubwa.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

23 Kwa kuwatuma wajumbe wako umemkashifu Bwana, wewe umesema, “Kwa magari yangu mengi ya vita, nimekwea vilele vya milima mpaka kilele cha Lebanoni. Nimekata mierezi yake mirefu, na misonobari mizurimizuri; nimeingia mpaka ndani yake na ndani ya misitu yake mikubwa.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

23 Kwa kuwatuma wajumbe wako umemkashifu Bwana, wewe umesema, “Kwa magari yangu mengi ya vita, nimekwea vilele vya milima mpaka kilele cha Lebanoni. Nimekata mierezi yake mirefu, na misonobari mizurimizuri; nimeingia mpaka ndani yake na ndani ya misitu yake mikubwa.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

23 Kupitia kwa wajumbe wako umelundika matukano juu ya Bwana. Nawe umesema, “Kwa magari yangu mengi ya vita, nimepanda juu ya vilele vya milima, vilele vya juu sana katika Lebanoni. Nami nimeiangusha mierezi yake mirefu, misunobari yake iliyo bora sana. Nimefikia sehemu zake zilizo mbali sana, misitu yake iliyo mizuri sana.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

23 Kupitia kwa wajumbe wako umelundika matukano juu ya Bwana. Nawe umesema, “Kwa magari yangu mengi ya vita, nimepanda juu ya vilele vya milima, vilele vya juu sana katika Lebanoni. Nami nimeiangusha mierezi yake mirefu, misunobari yake iliyo bora sana. Nimefikia sehemu zake zilizo mbali sana, misitu yake iliyo mizuri sana.

Tazama sura Nakili




2 Wafalme 19:23
15 Marejeleo ya Msalaba  

Mfalme wa Ashuru akawatuma jemadari wake, na mkuu wa matowashi, na kamanda wake, toka Lakishi, kwa mfalme Hezekia huko Yerusalemu, pamoja na jeshi kubwa. Nao wakakwea wakafika Yerusalemu. Na walipokwisha kufika, wakaja wakasimama karibu na mfereji wa birika la juu, lililo katika njia kuu ya kuuendea Uwanda wa Dobi.


Basi sasa, tafadhali mpe bwana wangu, mfalme wa Ashuru, dhamana, nami nitakupa farasi elfu mbili, ikiwa wewe kwa upande wako waweza kupandisha watu juu yao.


Yamkini BWANA, Mungu wako, atayasikia maneno yote ya kamanda huyu, ambaye mfalme wa Ashuru, bwana wake, amemtuma ili amtukane Mungu aliye hai; naye atayakemea hayo maneno aliyoyasikia BWANA, Mungu wako; kwa sababu hii inua dua yako kwa ajili ya mabaki yaliyobakia.


Akajenga minara tena nyikani, akachimba mabwawa mengi, maana alikuwa na ng'ombe tele; katika Shefela pia, na katika nchi tambarare; tena alikuwa na wakulima na watunza mizabibu milimani, na katika mashamba ya neema; maana yeye alipenda ukulima.


Tena akaandika waraka, kumtukana BWANA, Mungu wa Israeli, na kumwambia, akisema, Kama vile miungu ya mataifa wa nchi isivyowaokoa watu wao na mkono wangu, vivyo hivyo Mungu wa Hezekia hatawaokoa watu wake na mkono wangu.


Hawa wanataja magari na hawa farasi, Lakini sisi tutalitaja jina la BWANA, Mungu wetu.


Wao wameinama na kuanguka, Bali sisi tumeinuka na kusimama.


Kwa maana amesema, Kwa nguvu za mkono wangu nimetenda jambo hili, na kwa hekima yangu; maana mimi nina busara; nami nimeiondoa mipaka ya watu, nikaziteka akiba zao, nikawaangusha waketio juu ya viti vya enzi kama afanyavyo shujaa.


Na mkono wangu umezitoa mali za mataifa kama katika kiota cha ndege; na kama vile watu wakusanyavyo mayai yaliyoachwa, ndivyo nilivyokusanya dunia yote; wala hapana aliyetikisa bawa, wala kufumbua kinywa, wala kulia.


Naye atauteketeza utukufu wa msitu wake, na wa shamba lake linalositawi, tangu nafsi hata nyama ya mwili, itakuwa kama vile afapo mtu aliye mgonjwa.


Naam, ikajitukuza hata juu yake aliye mkuu wa jeshi hilo, ikamwondolea sadaka ya kuteketezwa ya daima, na mahali pa patakatifu pake pakaangushwa chini.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo