Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




2 Mambo ya Nyakati 14:2 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

2 Basi, Asa akafanya yaliyo mema, yaliyo ya adili, machoni pa BWANA, Mungu wake;

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

2 Asa alitenda yaliyokuwa mazuri na mema mbele ya Mwenyezi-Mungu, Mungu wake.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

2 Asa alitenda yaliyokuwa mazuri na mema mbele ya Mwenyezi-Mungu, Mungu wake.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

2 Asa alitenda yaliyokuwa mazuri na mema mbele ya Mwenyezi-Mungu, Mungu wake.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

2 Asa akatenda yaliyo mema na haki machoni pa Mwenyezi Mungu, Mungu wake.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

2 Asa akatenda yaliyo mema na haki machoni pa bwana Mwenyezi Mungu wake.

Tazama sura Nakili




2 Mambo ya Nyakati 14:2
15 Marejeleo ya Msalaba  

Basi, Asa akafanya yaliyo mema machoni pa Mungu, kama alivyofanya babaye Daudi.


Akawafukuza mahanithi katika nchi, akaziondoa sanamu zote walizozifanya baba zake.


Lakini mahali pa juu hapakuondoshwa; ila moyo wake Asa ulikuwa mkamilifu kwa BWANA siku zake zote.


Basi Abiya akalala na baba zake, wakamzika mjini mwa Daudi, akatawala Asa mwanawe mahali pake; katika siku zake nchi ikastarehe miaka kumi.


maana aliziondoa madhabahu za kigeni, na mahali pa juu, akazivunja nguzo, akayakatakata maashera;


Hata na Maaka mamaye Asa, mfalme akamwondolea cheo chake asiwe malkia, kwa kuwa amefanya sanamu ya kuchukiza kwa Ashera; basi Asa akaikata sanamu yake, akaiponda, akaiteketeza penye kijito cha Kidroni.


Ukainuliwa moyo wake katika njia za BWANA; na zaidi ya hayo akapaondoa mahali pa juu, na Maashera, katika Yuda.


Akaiendea njia ya Asa babaye, wala hakuiacha, akifanya yaliyo mema machoni pa BWANA.


Barua kutoka nabii Eliya ilimjia, ikisema, BWANA, Mungu wa Daudi baba yako, asema hivi, Kwa kuwa hukuziendea njia za Yehoshafati baba yako, wala njia za Asa mfalme wa Yuda;


Basi hayo yote yalipokwisha, Israeli wote waliokuwako wakatoka waende miji ya Yuda, wakazivunjavunja nguzo, wakayakatakata Maashera, wakabomoa mahali pa juu na madhabahu katika Yuda yote na Benyamini, katika Efraimu pia na Manase, hadi walipoviharibu vyote. Ndipo wana wa Israeli wote wakarudi, kila mtu kwa milki yake, mijini kwao.


Na hivyo ndivyo alivyofanya Hezekia katika Yuda yote; akatenda yaliyo mema, na ya adili, na uaminifu, mbele za BWANA, Mungu wake.


Akazibomoa madhabahu, akazipondaponda Maashera na sanamu kuwa mavumbi, akazikatakata sanamu zote za jua katika nchi yote ya Israeli, kisha akarejea Yerusalemu.


Usiisujudie miungu yao, wala kuitumikia; wala usitende mfano wa matendo yao; bali utaiangamiza kabisa, na nguzo zao utazivunja vipande vipande.


Kwa utakatifu na kwa haki Mbele zake siku zetu zote.


nanyi zivunjeni madhabahu zao, zibomoeni nguzo zao, na maashera yao yateketezeni kwa moto, na sanamu za kuchonga za miungu yao zikateni; na jina lao lifutilieni mbali na mahali hapo.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo