Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




1 Wakorintho 9:23 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

23 Nami nafanya mambo yote kwa ajili ya Injili ili kuishiriki pamoja na wengine.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

23 Nafanya haya yote kwa ajili ya Injili, nipate kushiriki baraka zake.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

23 Nafanya haya yote kwa ajili ya Injili, nipate kushiriki baraka zake.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

23 Nafanya haya yote kwa ajili ya Injili, nipate kushiriki baraka zake.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

23 Nafanya haya yote kwa ajili ya Injili, ili nipate kushiriki baraka zake.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

23 Nafanya haya yote kwa ajili ya Injili, ili nipate kushiriki baraka zake.

Tazama sura Nakili




1 Wakorintho 9:23
14 Marejeleo ya Msalaba  

Kwa kuwa mtu atakaye kuiponya nafsi yake, ataiangamiza, na mtu atakayeiangamiza nafsi yake kwa ajili yangu na kwa ajili ya Injili, huyu ataisalimisha.


Lakini iwapo matawi mengine yamekatwa, na wewe mzeituni mwitu ulipandikizwa kati yao, ukawa mshirika wa shina la mzeituni na unono wake,


Ikiwa wengine wanashiriki uwezo huu juu yenu, sisi si zaidi? Lakini hatukuutumia uwezo huo; bali twayavumilia mambo yote tusije tukaizuia Habari Njema ya Kristo.


Kwa wanyonge nilikuwa mnyonge, ili niwapate wanyonge. Nimekuwa hali zote kwa watu wote, ili kwa njia zote nipate kuwaokoa watu.


Je! Hamjui, ya kuwa wale washindanao kwa kupiga mbio, hupiga mbio wote, lakini apokeaye tuzo ni mmoja? Pigeni mbio namna hiyo, ili mpate.


Maana katika dhiki nyingi na taabu ya moyo niliwaandikia nikiwa na machozi mengi; si kwamba mhuzunishwe, bali mpate kujua upendo wangu nilio nao kwenu jinsi ulivyo mwingi.


ambao hata saa moja hatukujitia chini yao, ili kwamba kweli ya Injili ikae pamoja nanyi.


Kwa ajili ya hilo nastahimili mambo yote, kwa ajili ya wateule, ili wao nao waupate wokovu ule ulio katika Kristo Yesu, pamoja na utukufu wa milele.


Yampasa mkulima mwenye bidii ya kazi kuwa wa kwanza wa kupata fungu la mavuno.


Kwa hiyo, ndugu watakatifu, wenye kuushiriki mwito wa mbinguni, mtafakarini sana Mtume na Kuhani Mkuu wa maungamo yetu, Yesu,


Kwa maana tumekuwa washirika wa Kristo, kama tukishikamana na mwanzo wa uthabiti wetu kwa nguvu mpaka mwisho;


Nawasihi wazee walio kwenu, mimi niliye mzee, mwenzi wao, na shahidi wa mateso ya Kristo, na mshirika wa utukufu utakaofunuliwa baadaye;


hilo tuliloliona na kulisikia, tunawahubiria na ninyi; ili nanyi pia mpate kushirikiana nasi: na ushirika wetu ni pamoja na Baba, na pamoja na Mwana wake Yesu Kristo.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo