Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




1 Wafalme 12:16 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

16 Basi Israeli wote walipoona ya kuwa mfalme hakuwasikia, hao watu walimjibu mfalme, wakasema, Tuna sehemu gani katika Daudi? Wala hatuna urithi katika mwana wa Yese. Haya! Nendeni zenu hemani kwenu, enyi Israeli; sasa itunze nyumba yako mwenyewe, Ee Daudi. Hivyo Israeli wakaenda zao hemani kwao.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

16 Lakini watu wote wa Israeli walipoona kwamba mfalme hakuwajali, walimwambia, “Hatuna uhusiano wowote na Daudi! Hatuna sehemu yetu kutoka kwa huyo mwana wa Yese. Rudini nyumbani, enyi watu wa Israeli! Itunze nyumba yako mwenyewe, ee Daudi.” Hivyo, watu wa Israeli wakarudi makwao.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

16 Lakini watu wote wa Israeli walipoona kwamba mfalme hakuwajali, walimwambia, “Hatuna uhusiano wowote na Daudi! Hatuna sehemu yetu kutoka kwa huyo mwana wa Yese. Rudini nyumbani, enyi watu wa Israeli! Itunze nyumba yako mwenyewe, ee Daudi.” Hivyo, watu wa Israeli wakarudi makwao.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

16 Lakini watu wote wa Israeli walipoona kwamba mfalme hakuwajali, walimwambia, “Hatuna uhusiano wowote na Daudi! Hatuna sehemu yetu kutoka kwa huyo mwana wa Yese. Rudini nyumbani, enyi watu wa Israeli! Itunze nyumba yako mwenyewe, ee Daudi.” Hivyo, watu wa Israeli wakarudi makwao.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

16 Israeli wote walipoona kuwa mfalme amekataa kuwasikiliza, wakamjibu mfalme: “Je, tuna fungu gani kwa Daudi? Tuna urithi gani kwa mwana wa Yese? Nendeni kwenye mahema yenu, ee Israeli! Angalia nyumba yako mwenyewe, ee Daudi!” Hivyo Waisraeli wakaenda kwenye mahema yao.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

16 Israeli wote walipoona kuwa mfalme amekataa kuwasikiliza, wakamjibu mfalme: “Tuna fungu gani kwa Daudi? Sisi hatuna urithi kwa mwana wa Yese. Nendeni kwenye mahema yenu, ee Israeli! Angalia nyumba yako mwenyewe, ee Daudi!” Hivyo Waisraeli wakaenda kwenye mahema yao.

Tazama sura Nakili




1 Wafalme 12:16
32 Marejeleo ya Msalaba  

Mjumbe akamfikia Daudi, akasema, Mioyo ya watu wa Israeli inashikamana na Absalomu.


Daudi akamwambia Abishai, na watumishi wake wote, Angalieni, huyu mwanangu, aliyetoka viunoni mwangu, anautafuta uhai wangu; sembuse Mbenyamini huyu? Mwacheni alaani, kwa sababu BWANA ndiye aliyemwagiza.


Basi ilitukia ya kwamba kulikuwapo mtu asiyefaa, jina lake akiitwa Sheba, mwana wa Bikri, Mbenyamini; naye akapiga tarumbeta, akasema, Sisi hatuna sehemu katika Daudi, wala hatuna urithi katika mwana wa Yese; nendeni kila mtu hemani kwake, enyi Israeli.


Kwa hiyo BWANA akamwambia Sulemani, Kwa kuwa umefanya hayo, wala hukuyashika maagano yangu, na sheria zangu nilizokuamuru, hakika nitaurarua ufalme usiwe wako, nami nitampa mtumishi wako.


Lakini sitauondoa ufalme wote pia; nitampa mwana wako kabila moja, kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu, na kwa ajili ya Yerusalemu niliouchagua.


Lakini sitauondoa ufalme wote katika mkono wake; bali nitamfanya awe mkuu siku zote za maisha yake, kwa ajili ya mtumishi wangu Daudi niliyemchagua kwa maana alizishika amri zangu na sheria zangu,


ila nitauondoa ufalme katika mkono wa mwanawe, nami nitakupa wewe makabila kumi.


Nami nitampa mwana wake kabila moja, ili Daudi, mtumishi wangu, apate kuwa na taa siku zote mbele zangu katika Yerusalemu, mji ule niliouchagua niweke jina langu huko.


Tena nitawatesa wazao wa Daudi kwa sababu hii, lakini si daima.


Akasema, Niliwaona Waisraeli wote wametawanyika milimani, kama kondoo wasio na mchungaji. BWANA akasema, Hawa hawana bwana; na warudi kila mtu nyumbani kwake kwa amani.


Ikapigwa mbiu jeshini, jua likichwa, kusema, Kila mtu aende mjini kwake, na kila mtu shambani kwake.


Basi Israeli wote walipoona ya kuwa mfalme hawasikilizi, watu wakamjibu mfalme, wakasema, Tuna sehemu gani katika Daudi? Wala hatuna urithi katika mwana wa Yese; kila mtu aende zake hemani, enyi Israeli, sasa itunze nyumba yako mwenyewe ewe Daudi. Basi wakaenda zao Israeli wote hemani kwao.


Hapo nitamchipushia Daudi pembe, Na taa nimemtengenezea masihi wangu.


Maana hasira ya binadamu itakusifu, Masalio ya hasira utajifunga kama mshipi.


Jawabu la upole hugeuza hasira; Bali neno liumizalo huchochea ghadhabu.


BWANA ataleta juu yako, na juu ya watu wako, na juu ya nyumba ya baba yako, siku zisizokuja bado, tangu siku ile aliyoondoka Efraimu kutoka katika Yuda; yaani, mfalme wa Ashuru.


Kisha watu wa nyumba ya Daudi wakaambiwa kwamba Shamu wamefanya mapatano na Efraimu. Na moyo wake ukataharuki, na moyo wa watu wake, kama miti ya mwituni itikiswavyo na upepo.


ndipo agano langu nililolifanya na Daudi, mtumishi wangu, laweza kuvunjika, hata asiwe na mwana wa kumiliki katika kiti chake cha enzi; tena agano langu nililofanya na Walawi makuhani, wahudumu wangu, laweza kuvunjika.


Na wewe mwanadamu, twaa kijiti kimoja; ukaandike juu yake, Kwa Yuda, na kwa wana wa Israeli wenzake; kisha, twaa kijiti cha pili; ukaandike juu yake, Kwa Yusufu, kijiti cha Efraimu, na kwa nyumba yote ya Israeli wenzake;


Na ufalme ukifitinika juu ya nafsi yake, ufalme huo hauwezi kusimama;


Lakini watu wa mji wake walimchukia, wakatuma wajumbe kumfuata na kusema, Hatumtaki huyu atutawale.


Tena, wale adui zangu, wasiotaka niwatawale, waleteni hapa muwachinje mbele yangu.


Petro akamwambia, Wewe hutaniosha miguu kamwe. Yesu akamwambia, Nisipokuosha, huna shirika nami.


wala hawakuifanyia mema nyumba ya Yerubaali, yaani Gideoni, licha ya hayo mema yote aliyowafanyia Waisraeli.


Naye Gaali mwana wa Ebedi akasema, Abimeleki ni nani, na sisi wa Shekemu ni nani, hata tukamtumikie yeye? Je, huyu mwana wa Yerubaali na Zebuli afisa wake hawakuwatumikia watu wa Hamori babaye Shekemu? Basi, kwa nini tumutumikie?


Tufuate:

Matangazo


Matangazo