Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




1 Wafalme 12:13 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

13 Mfalme akawajibu watu wale kwa ukali, akaliacha shauri lile wazee walilompa;

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

13 Mfalme akawajibu watu hao kwa ukali, akapuuza shauri alilopewa na wazee,

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

13 Mfalme akawajibu watu hao kwa ukali, akapuuza shauri alilopewa na wazee,

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

13 Mfalme akawajibu watu hao kwa ukali, akapuuza shauri alilopewa na wazee,

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

13 Mfalme akawajibu watu kwa ukatili. Alikataa ushauri alilopewa na wazee,

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

13 Mfalme akawajibu watu kwa ukatili. Akikataa shauri alilopewa na wazee,

Tazama sura Nakili




1 Wafalme 12:13
21 Marejeleo ya Msalaba  

Naye Abramu akamwambia Sarai, Tazama, mjakazi wako yu mikononi mwako, mtendee lililo jema machoni pako. Sarai akamtesa, naye akakimbia kutoka mbele yake.


Mtu yule aliye bwana wa nchi alisema nasi kwa maneno makali, akatufanya tu wapelelezi wa nchi.


Yusufu akawaona nduguze, akawatambua, lakini alijifanya kama mgeni kwao. Akasema nao kwa maneno makali, akawaambia, Mmetoka wapi ninyi? Wakasema. Tumetoka nchi ya Kanaani, ili tununue chakula.


Hao watu wa Israeli wakawajibu watu wa Yuda, wakasema, Sisi tunazo sehemu kumi katika mfalme, tena tunayo haki yetu katika Daudi zaidi kuliko ninyi; mbona basi ninyi mmetudharau sisi, msitake ushauri wetu kwanza katika kumrudisha tena mfalme wetu? Na maneno ya watu wa Yuda yakawa makali kuliko maneno ya watu wa Israeli.


Basi, Yeroboamu na watu wote wakamfikia Rehoboamu siku ya tatu, kama mfalme alivyoamuru, akisema, Mnirudie siku ya tatu.


akawajibu kama vile walivyomshauri vijana, akasema, Baba yangu alilifanya zito kongwa lenu, bali mimi nitaongeza kongwa lenu; baba yangu aliwapiga kwa mijeledi, bali mimi nitawapigeni kwa nge.


Farao akamwambia Musa, Nenda zako, ujiangalie, usinione uso tena; kwani siku hiyo utakayoniangalia uso wangu utakufa.


Farao akasema, BWANA ni nani, hata niisikilize sauti yake, na kuwapa Israeli ruhusa waende zao? Mimi simjui BWANA, wala sitawapa Israeli ruhusa waende zao.


Kinywa chake mwenye haki ni chemchemi ya uzima; Bali jeuri hufunika kinywa chake mtu mwovu,


Midomo ya mwenye haki huyajua yatakayokubaliwa; Bali kinywa chao wasio haki hunena ukaidi.


Nenda pamoja na wenye hekima, nawe utakuwa na hekima; Bali rafiki wa wapumbavu ataumia.


Jawabu la upole hugeuza hasira; Bali neno liumizalo huchochea ghadhabu.


Maskini hutumia maombi; Bali tajiri hujibu kwa ukali.


Maneno ya kinywa chake mwenye hekima yana neema; Bali midomo ya mpumbavu itammeza nafsi yake.


Naye ni nani ajuaye kama huyo atakuwa mwenye hekima au mpumbavu? Hata hivyo atatawala juu ya kazi yangu yote niliyojishughulisha nayo, ambamo ndani yake mimi nimeonesha hekima chini ya jua. Hayo nayo ni ubatili.


Lakini hekima itokayo juu, kwanza ni safi, tena ni ya amani, ya upole, tayari kusikiliza maneno ya watu, imejaa rehema na matunda mema, haina fitina, haina unafiki.


Basi Daudi akamwambia Yonathani, Ni nani atakayeniambia, ikiwa baba yako amekujibu maneno makali?


Tufuate:

Matangazo


Matangazo