Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Yohana 8:29 - New Testament in Swahili (Zanzibar) Revised Edition 1921

29 Nae aliyenipeleka yu pamoja nami; Baba hakuniacha peke yangu: kwa sababu mimi nafanya siku zote yampendezayo.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

29 Yule aliyenituma yuko pamoja nami; yeye hakuniacha peke yangu kwani nafanya daima yale yanayompendeza.”

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

29 Yule aliyenituma yuko pamoja nami; yeye hakuniacha peke yangu kwani nafanya daima yale yanayompendeza.”

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

29 Yule aliyenituma yuko pamoja nami; yeye hakuniacha peke yangu kwani nafanya daima yale yanayompendeza.”

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

29 Yeye aliyenituma yu pamoja nami; hajaniacha, kwa kuwa siku zote nafanya mapenzi yake.”

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

29 Yeye aliyenituma yu pamoja nami, hajaniacha, kwa kuwa siku zote nafanya mapenzi yake.’ ”

Tazama sura Nakili




Yohana 8:29
25 Marejeleo ya Msalaba  

Alipokuwa akisema, wingu jeupe likawatia uvuli; sauti ikatoka katika lile wingu, ikinena, Huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, niliyependezwa nae; msikieni yeye.


Yesu akajibu, akamwambia, Hayo yaache sasa: kwa kuwa hivi imetupasa kutimiza haki yote. Bassi akamwacha.


na sauti toka mbinguni ikinena, Huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, ninaependezwa nae.


lakini ulimwengu ujue ya kuwa nampenda Baba; na, kama Baba alivyoniamuru, ndivyo nifanyavyo. Ondokeni, tufoke huku.


Mkizishika amri zangu, mtakaa katika pendo langu; kama mimi nilivyozishika amri za Baba yangu, na kukaa katika pendo lake.


Saa inakuja, naam, imekwisha kuja, mtatawanyika killa mmoja kwa mambo yake, mtaniacha mimi peke yangu; wala mimi si peke yangu, kwa kuwa Baba yupo pamoja nami.


Mimi nimekutukuza duniani. Kazi ile uliyonipa niifanye nimeimaliza.


Yesu akawaambia, Chakula changu ndicho hiki, niyatende mapenzi yake aliyenipeleka nikaimalize kazi yake.


Mimi siwezi kufanya neno kwa nafsi yangu: kama nisikiavyo ndivyo nihukumuvyo, na hukumu yangu ina haki: kwa sababu siyatafuti mapenzi yangu mwenyewe, bali mapenzi yake Baba aliyenipeleka.


Kwa kuwa sikushuka kutoka mbinguni illi niyafanye mapenzi yangu, hali mapenzi yake aliyenipeleka.


Na nijapohukumu, hukumu yangu ni kweli, kwa kuwa mimi si peke yangu bali mimi na Baba aliyenipeleka.


Lakini Bwana alisimama pamoja nami akanitia nguvu, illi kwa kazi yangu ule ujumbe utangazwe kwa utimilifu, mataifa wrote wakasikie; nikaokolewa katika kanwa la simba.


Bwana Yesu Kristo awe pamoja na roho yako. Neema na iwe nanyi. Amin.


Kwa kuwa hatuna kuhani mkuu asiyeweza kuyachukua mambo yetu ya udhaifu; bali yeye alijuribiwa sawa sawa na sisi katika mambo yote, bila dhambi.


Maana ilipendeza sisi tuwe na kuhani mkuu wa namna hii, aliye mtakatifu, asiokuwa na uovu, asiokuua na waa lolote, aliyetengwa na wakosaji, aliyekuwa juu kuliko mbingu;


WATOTO wangu wadogo, nawaandikia haya illi msitende dhambi. Na ijapo mtu akatenda dhambi tuna Mwombezi kwa Baba, Yesu Kristo mwenye haki,


na lo lote tuombalo, twalipokea kwake, kwa kuwa twazishika amri zake, na kuyatenda yapendezayo machoni pake.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo