Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Yohana 1:51 - New Testament in Swahili (Zanzibar) Revised Edition 1921

51 Akamwambia, Amin, amin, nakuambieni, Tangu sasa mtaziona mbingu zimefunguka, na malaika wa Mungu wakipanda, wakishuka juu ya Mwana wa Adamu.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

51 Yesu akaendelea kusema, “Nawaambieni kweli, mtaona mbingu zinafunguka na malaika wa Mungu wakipanda na kushuka juu ya Mwana wa Mtu.”

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

51 Yesu akaendelea kusema, “Nawaambieni kweli, mtaona mbingu zinafunguka na malaika wa Mungu wakipanda na kushuka juu ya Mwana wa Mtu.”

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

51 Yesu akaendelea kusema, “Nawaambieni kweli, mtaona mbingu zinafunguka na malaika wa Mungu wakipanda na kushuka juu ya Mwana wa Mtu.”

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

51 Ndipo akawaambia, “Amin, amin nawaambia, ninyi mtaona mbingu ikifunguka na malaika wa Mungu wakipanda na kushuka juu ya Mwana wa Adamu.”

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

51 Ndipo akawaambia, “Amin, amin nawaambia, ninyi mtaona mbingu ikifunguka na malaika wa Mungu wakipanda na kushuka juu ya Mwana wa Adamu.”

Tazama sura Nakili




Yohana 1:51
55 Marejeleo ya Msalaba  

Hatta atakapokuja Mwana wa Adamu katika utukufu wake, na malaika watakatifu wote pamoja nae, ndipo atakapoketi katika kiti cha utukufu wake:


Mwana wa Adamu aenda zake, kama alivyoandikiwa: lakini ole wake mtu yule ambae Mwana wa Adamu anasalitiwa nae! Ingekuwa kheri kwake mtu yule kama asingalizaliwa.


Nae Yesu alipokwisha kubatizwa marra akapanda kutoka majini: mbingu zikamfunukia, akamwona Roho ya Mungu akishuka kama hua, akija juu yake:


Kisha Shetani akamwacha; wakaja malaika wakamtumikia.


Yesu akamwambia, Mbweha wana matundu, na ndege za anga vituo; bali Mwana wa Adamu hana pa kulaza kichwa chake.


Lakini illi mjue ya kuwa Mwana wa Adamu yuna mamlaka katika dunia kuondoa dhambi, (amwambia yule mgonjwa wa kupooza) Ondoka, ujitwike kitanda chako, ukaende nyumbani kwako.


Marra akapanda kutoka majini, akaona mbingu zinapasuka, na Roho, kwa mfano wa hua, akishuka juu yake;


Yesu akasema, Mimi ndio yeye, nanyi mtamwona Mwana wa Adamu ameketi mkono wa kuume wa nguvu, akija na mawingu ya mbingu.


Ghafula hiyo walikuwapo pamoja na yule malaika wengi wa jeshi la mbinguni, wakimsifu Mungu, wakisema,


Malaika wa Bwana akawatokea, utukufu wa Bwana ukawangʼaria: wakaingiwa na khohi nyingi.


Akamtokea malaika toka mbinguni akimtia nguvu.


Lakini tangu sasa Mwana wa Adamu atakuwa ameketi mkono wa kuume wa ukuu wa Mungu.


Ikawa wangali wakishangaa kwa haya, kumbe! watu wawili wakisimama karibu yao, wamevaa nguo za kumetameta.


Na watu wote walipokwisha kubatizwa, na Yesu nae akiisha kubatizwa, na akisali, mbingu zilifunuka.


Yesu akajibu, akamwambia, Kwa sababu nalikuambla, Nalikuona chini ya mtini, waamini? Utaona mambo makubwa kuliko haya.


AMIN, amin, nawaambieni, asiyeingia kwa mlango katika zizi la kondoo, lakini apanda penginepo, huyu ni mwizi na mnyangʼanyi.


Bassi Yesu aliwaamhia tena, Amin, amin, nawaambieni, Mimi ndimi niliye mlango wa kondoo;


Amin, amin, nawaambieni, Mtumwa si mkuu kuliko bwana wake: wala mtume si mkuu kuliko yeye aiiyempeleka.


Yesu akamjibu, Je! uzima wako utauweka kwa ajili yangu? Amin, amin, nakuambia, Jogoo hatawika hatta utakapokuwa umenikana marra tatu.


Amin, amin, nawaambieni, Aniaminiye mimi, kazi nizifanyazo mimi na yeye atazifanya; atafanya na kubwa kuliko hizi, kwa kuwa nashika njia kwenda kwa Baba.


Amin, amin, nawaambieni, Ninyi mtalia, na kuomboleza, bali, ulimwengu utafurahi: ninyi mtahuzunishwa, lakini huzuni yenu itageuka kuwa furaha,


Na siku ile hamtaniuliza neno. Amin, amin, nawaambieni, Mkimwomba Baba neno kwa jina langu atawapeni.


Amin, amin, nakuambia, Ulipokuwa kijana, ulikuwa ukijifunga, ukienda ulikotaka; utakapokuwa mzee, utanyosha mikono yako, na mwingine atakufunga, atakuchukua usikotaka.


Yesu akajibu, akamwambia, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa marra ya pili, hawezi kuuona ufalme wa Mungu.


Yesu akajibu, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa kwa maji na Roho, hawezi kuuingia ufalme wa Mungu.


Bassi Yesu akajibu, akawaambia, Amin, amin, nawaambieni, Mwana hawezi kutenda neno kwa nafsi yake, illa lile amwonalo Baba analitenda; kwa maana yote atendayo yeye, hayo na Mwana ayatenda vilevile.


akampa mamlaka ya kufanya hukumu kwa sababu yu Mwana wa Adamu.


Yesu akawajibu, akasema, Amin, amin, nawaambieni, Mnanitafuta, si kwa sababu mliona ishara, bali kwa sababu mlikula ile mikate, mkashiba.


Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambieni, Siye Musa aliyewapa mkate ule kutoka mbinguni, bali Baba yangu anawapa mkate ule utokao mbinguni ulio wa kweli.


Amin, amin, nawaambieni, Yeye aniaminiye mimi ana uzima wa milele.


Bassi Yesu akawaambia, Amin, amin, nsiwaambieni. Msipoila nyama yake Mwana wa Adamu na kuinywa damu yake, hamna uzima ndani jemi.


Yesu akawajibu, Amin, amin, nawaambieni, Killa atendae dhambi, ni mtumwa wa dhambi.


Amin, amin, nawaambieni, Mtu akilishika neno langu, hataona mauti kabisa hatta milele.


Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambieni, Kabla Ibrahimu hajakuwapo, Mimi nipo.


na chombo kikimshukia kama nguo kubwa, kinatelemshwa kwa pembe zake nne hatta inchi.


Akasema, Tazama! naona mbingu zimefunuliwa, na Mwana wa Adamu amesimama mkono wa Mungu.


na kuwalipa ninyi mteswao raha pamoja na sisi wakati wa kufunuliwa kwake Bwana Yesu kutoka mbinguni pamoja na malaika wa uweza wake,


watakaoadhibiwa kwa uharibifu wa milele, kutengwa na uso wa Bwana na na utukufu wa nguvu zake,


Na bila shaka siri ya utawa ni kuu. Mungu alidhibirishwa katika mwili, alihesabiwa kuwa na wema katika roho, alionekana na malaika, alikhubiriwa katika mataifa, aliaminiwa katika ulimwengu, alichukuliwa juu katika utukufu.


Hawo wote si roho zitumikazo, wakitumwa kuwakhudumu wale watakaourithi wokofu?


Na Enok, wa saba baada ya Adamu, alitoa maneno ya unabii juu ya hawo, akisema, Angalia, Bwana alikuja na elfu kumi za watakatifu wake,


Nikaziona mbingu zimefunuka, na tazama farasi mweupe, nae aliyempanda, aitwae Mwaminifu na wa kweli, nae kwa haki ahukumu na kufanya vita.


BAADA ya haya naliona, na tazama mlango ukafunguka mbinguni, na sauti ya kwanza niliyoisikia kama sauti ya baragumu ikinena nami, ikisema, Panda hatta huku, nami nitakuonyesha mambo ambayo hayana buddi kuwa baada ya bayo.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo